Tuesday, December 31, 2013

Boban ni mchezaji halali wa CUSC

 Kikosi cha maangamizi cha CUSC....

 Hiki ni kipande cha gazeti la leo Jumatano Januari 1,2014 gazeti Mtanzania kuhusu habari za Boban.



Haruna Moshi, akimiliki mpira katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha wakati akiitumikia CUSC kwenye mechi yake ya kwanza ligi kuu na Wagosi wa Kaya. Ilikuwa ni mechi dhidi ya Oljoro JKT, ambapo CUSC iliibuka na ushindi wa mabao 2-0.
 
Ndugu zangu,
WIKI hii kumekuwa na habari za upotoshaji juu ya kutimuliwa kwa kiungo mshambuliaji wa Coastal Union ‘Wagosi wa Kaya’, Haruna Moshi ‘Boban’.
Ninaziita habari za upotoshaji kwasababu hazina ukweli, na mara nyingine mtu anaweza kuenda mbali zaidi na kufikiri kuwa kuna hujuma zinafanyika dhidi ya timu yetu ili wachezaji wasicheze kwa moyo wakati wa mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Tanzania Bara, unaotarajiwa kuanza Januari 25 mwaka huu.
Gazeti moja la michezo, jina tunalihifadhi limeripoti likimnukuu kiongozi mmoja wa Wagosi wa Kaya, jina pia tunalihifadhi kutokana na heshima yake; kuwa Coastal Union haina mpango wa kumuongezea mkataba ‘Boban’ baada ya kumalizika miezi sita ijayo kwasababu za utovu wa nidhamu.
Habari hizo hazina ukweli kwasababu hakuna kikao kilichokaliwa kujadili mustakabali wa mchezaji huyo. Ni kweli Boban, hajaripoti kambini mpaka sasa; lakini uongozi wa juu akiwemo meneja wa timu unazo taarifa za mchezaji huyo.
Kuwa na nidhamu ama kutokuwa na nidhamu, kumtimua ama kumuacha mchezaji, wanaoamua hayo ni uongozi wa juu kupitia kamati zake ndogondogo kama za mashindano, usajii na nidhamu. Na si mtu mmoja mmoja.
Hivyo kwa niaba ya Mwenyekiti wa Coastal Union, Hemed Hilal ‘Aurora’ timu inaomba radhi wanachama wa CUSC, kutokana na kuumizwa kwa namna moja ama nyingine na taarifa hizo za upotoshwaji.
Wagosi wa Kaya, bado wana mkataba wa miezi sita na Boban, kuongezewa ama kutoongezewa mkataba suala hilo litajadiliwa kati ya mchezaji na viongozi pale utakapofika ukingoni.
HAFIDH A. KIDO
MSEMAJI CUSC
JANUARI 1, 2014
DAR ES SALAAM, TANZANIA

Friday, December 27, 2013

Safari na mechi ya Ifakara dhidi ya Techfort...




 Kutoka kushoto, Katibu wa Coastal Union, Kassim Siagi, Kocha msaidizi Ally jangalu, Kocha Mkuu Yusuf Chipo na meneja wa U20 Abdul Ubinde.

 Mwalimu Yusuf Chipo, akizungumza na meneja wa U20, Abdul Ubinde kabla ya mechi kuanza..


 Abdullah Othman 'Sheikh Dullah' akijaribu kumtoka beki wa Techfort.



 Bao la kwanza lilianzia hapa, Danny alipenyezewa mpira, akamzidi nguvu beki wa Techfort, na kufunga.

 Bao la kwanza liliingua kimiani dakika ya 53 kipindi cha pili, liliingizwa kimiani na Danny Lyanga.

                        Masumbuko Kenneth katika moja ya harakati zake uwanjani juzi.

 Mohammed Miraji akishangilia bao la pili lililoingia dakika ya 90.



Baada ya mechi, wakazi wa Ifakara walilizunguka gari Coastal Union kuona wachezaji.........
 
Desemba 25, Coastal Union ilishuka dimbani kucheza mechi ya kujipima nguvu na Techfort FC, mabingwa wa Soka Mkoa wa Morogoro. Matokeo ni ushindi kwa Coastal Union 2-0. Mabao yalifungwa na Danny Lyanga na Mohammed Miraji.

Baada ya hapo timu ilirejea leo mjini Tanga, ambapo leo saa tisa Alasiri katika uwanja wa Gymkana timu itaendelea na mazoezi. Nawashauri walio mjini Tanga waende kuwaangalia vijana wamekuwa vizuri sana.

Aidha jana mwalimu Yusuf Chipo akishirikiana na mwalimu msaidizi Ally Jangalu, walimteua Juma Said Nyosso 'Baba Moza' kuwa nahodha mpya wa Coastal Union akishirikiana na Mbwana Khamis Kibacha.

Uteuzi huo umeanza mara moja siku ya juzi, na kuhusu nahodha wa zamani Jerry Santo, hakuna uhusiano wowote kati ya kuchelewa kwake kuwasili kambini na kuvuliwa unahodha. Bali mwalimu ameona Nyoso, kwa kipindi hiki anafaa kuwa nahodha kutokana na uzoefu wake katika ligi ya Tanzania na ana ufahamu mkubwa kwa wachezaji wa timu nyingine hasa katika masuala ya uwanjani.

Kutowasili kambini kwa Haruna Moshi 'Boban' na Jerry Santo, mwalimu na uongozi mzima wa Coastal Union unazo taarifa. Na wachezaji hao waliomba ruhusa kwa uongozi kuwa watachelewa kwa sababu za kifamilia na uongozi unafahamu hivyo na umewakubalia.

Wataungana na timu ziku yoyote kuanzia kesho kujiandaa na safari ya Oman, ambayo imepangwa kufanyika kabla ya taerehe 6 Januari. Timu itakaa huko kwa siku 14. Itacheza mechi si chini ya tano lakini si zaidi ya sita kwa muda wote watakaokaa huko.

Baada ya hapo watarejea nchini kabla ya Januari 25, ambapo watakuwa na mechi ya ufunguzi wa Ligi mzunguko wa pili dhidi ya Oljoro JKT katika uwanja wa Mkwakwani saa kumi alasiri.

HAFIDH KIDO
MSEMAJI- COASTAL UNION
27 DEC, 2013
TANGA, TANZANIA

Monday, December 2, 2013

Angalia mechi ya fainali Yanga walivyolala 2-0....





 Meneja Ubinde akibebwa na wanawe...

Mtenje Juma Albano



COASTAL UNION
DECEMBA 2, 2013
DAR ES SALAAM, TANZANIA

Kikombe cha Uhai chaenda Tanga

 Kikosi cha maangamizi kutoka kushoto waliosimama Nzara Ndaro, Gereza Mwaita, Ally Nassor, Mohammed Issa, Mohammed Rajab, Fikirini Selemani. Waliopiga magoti kutoka kushoto, Omar Mohammed, Mtenje Albano, Ally Kipanga, Ayoub Masudi na Mohammed Omar (Chizungu).








COASTAL UNION
2 DECEMBA, 2013
DAR ES SALAAM, TANZANIA

Thursday, November 28, 2013

Coastal Union hiyooooo Fainali Uhai Cup. Kwa mara ya pili mfululizo









COASTAL Union, wameudhihirishia umma kuwa mwaka jana walipoingia fainali ya Uhai Cup, hawakubahatisha baada ya kuwatoa Azam FC, katika mechi ya leo hatua ya nusu fainali ya kombe hilo uwanja wa Chamazi, Azam Complex jioni hii.

Kufungwa kwa Azam FC bao 1-0, imekuwa pigo kubwa kwa timu hiyo hasa ikizingatiwa katika mechi ya ufunguzi walitandikwa mabao 2-1 kwenye uwanja wa Karume Ilala jijini.

"Sisi kwa sasa tumeshafuta rekodi yao ya kutufunga mara mbili, walitufunga katika mechi ya fainali michuano hii hii mwaka jana baada ya dakika tisini wakatufunga kwa matuta. Baadaye mwaka huu katika michuano ya Rollingstone jijini Arusha wakatutoa kwa matuta kwenye hatua ya nusu fainali.

"Sasa sisi tumelipiza vipigo vya katika michuano hii hii, wao walitufunga katika michuano miwili tofauti tena kwa matuta, lakini sisi tumewafunga mara mbili mfululizo kwa tofauti ya wiki moja tu tena kwa dakika tisini," alijitapa beki wa kushoto wa Coastal Union Ayoub Masudi.

Bao la Wagosi lilipatikana dakika ya 32 kipindi cha kwanza baada ya Ally Nassor 'Ufudu' kukimbia na mpira kitokea katikati na kumpenyezea Mohammed Rajab ambaye aliwekwa kati na mabeki wawili wa Azam FC, lakini akawashinda nguvu na mbio, mwisho akabaki yeye na kipa, akapiga shuti hafifu ambalo lilipita juu ya goikipa huyo ambaye aliinua macho bila msaada huku mpira ukitinga wavuni.

Baada ya hapo Coastal Union, walicheza mpira wa kasi na kuonana hali iliyozidi kuwachanganya Azam ambao walikuwa wakizomewa na uwanja mzima.

Mpaka mapumziko matokeo yalibaki hivyohivyo 1-0, kipindi cha pili Azam walirudi na ari wakacheza nusu uwanja kwa takriban dakika ishirini, Coastal Union walionekana kupoteza mwelekeo na hawajui cha kufanya.

Hali ilizidi kuwa mbaya baada ya kocha wa Azam kuingiza wachezaji wannne ndani ya dakika tano, hali iliyowafanya Wagosi kuzidi kuelemewa na kuamua kurudi nyuma kulnda lango badala ya kuongeza bao la pili.

Awali wakati kipindi cha pili kinaanza Kocha Joseph Lazaro alimtoa Mohammed Issa 'Banka' na kumuingiza Hussein Amir 'Zola. baadaye ilipotimia dakika ya 40 alitoka Mahadhi Juma, ambaye leo alicheza chini ya kiwango na kuingia Dihile Said, kabla ya mchezo kuisha aliingia Ramadhan Juma 'Batisata' na kutoka Mohammed Rajabu.

Coastal Union dakika kumi za mwisho walicheza soka la kuvutia na kujiamini kiasi walishangiliwa na uwanja mzima.

Mechi ya fainali itakayochezwa Jumapili wiki hii saa tisa alasiri uwanja wa Chamazi, inasubiri mshindi kati ya Yanga na Mtibwa Sugar ambayo itapigwa kesho uwanja wa Chamazi.

COASTAL UNION
28 NOVEMBA, 2013
DAR ES SALAAM, TANZANIA