Tuesday, April 30, 2013

Mechi kati ya Coastal Union na Yanga kuvutia wengi uwanja wa taifa kesho.

Makocha wa Coastal Union Kocha mkuu Hemed Morocco (mwenye kofia), Kocha msaidizi Ally Kido (katikati), na kocha wa magolikipa Juma Pondamali 'Mensah' wakijadiliana kitu.


Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inaendelea katika raundi yake ya 25 kesho (Mei Mosi) kwa mechi tano zitakazochezwa katika miji ya Dar es Salaam, Turiani, Morogoro na Mlandizi.

Licha ya kuwa tayari Yanga imetawazwa kuwa mabingwa wa VPL msimu huu (2012/2013), mechi dhidi ya Coastal Union itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni moja kati ya zitakazovuta macho na masikio ya washabiki wa mpira wa miguu nchini.

Mechi hiyo namba 172 itachezeshwa na mwamuzi Simon Mberwa kutoka Pwani akisaidiwa na Said Mnonga na Charles Chambea wote wa Mtwara wakati mwamuzi wa mezani atakiwa Hashim Abdallah wa Dar es Salaam. Kamishna wa mechi hiyo ni David Lugenge kutoka Iringa.

Viingilio katik mechi hiyo itakayoanza saa 10.15 jioni ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, sh. 8,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 kwa VIP C na B wakati VIP A itakuwa sh. 20,000. Tiketi zitauzwa uwanjani siku ya mchezo.

Mtibwa Sugar itakuwa mwenyeji wa African Lyon katika mechi namba 170 itakayochezeshwa na mwamuzi Dominic Nyamisana wa Dodoma kwenye Uwanja wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro. Nayo Kagera Sugar iliyo katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi hiyo itakuwa mgeni wa Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi, Dar es Salaam na wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 7,000 uko tayari kwa mechi kati ya JKT Ruvu na Tanzania Prisons. Nayo Ruvu Shooting itakuwa nyumbani kwenye uwanja wake Mabatini ulioko Mlandizi, Pwani kuikabili Oljoro JKT kutoka Arusha.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Aprili 30, 2013

Friday, April 26, 2013

Daniel Lyanga wa Coastal Union atimiza bao la saba katika msimu huu.

Daniel Lyanga wa Copastal Union (kulia) aikokota mpira mbele ya mchezaji wa Azam FC.

SULUHU ya bao moja kwa moja katika mechi ya soka ligi kuu Vodacom Tanzania bara leo kati ya Coastal Union na Azam FC uwanja wa mkwakwani Tanga imesadia timu ya Yanga kutangaza ubingwa wakiwa na mechi mbili mkononi.

Yanga ambao wana point 56 walikuwa wanataka point moja tu waweze kutangazwa mabingwa wa soka Tanzania bara lakini kwa Azam FC kutoa suluhu ya 1-1 na Coastal Union leo kumewafanya wana lambalamba hao kuvuna point moja hivyo kupata idadi ya point 48 kitu ambacho kwa mech mbili walizobakisha hawawezi kufikia pont 56 ambazo Yanga tayari wanazo na hakuna timu yoyote yenye uwezo wa kuzifikia.

Mchezaji wa wagosi wa kaya Daniel Lyanga aliyeingia kipindi cha pili kwa kuchukua nafasi ya Suleiman Kassim 'Selembe' ndiye aliyelazimisha suluhu hiyo mnamo dakika ya 71 ya mchezo ambayo ilikuwa ni dakika moja tu tangu aingie dakika ya 70 ambapo mpira wa kwanza kuugusa ikawa shangwe kwa mashabki wa Coastal na kutimiza goli la saba kwa msimu huu.

Awali mwamuzi wa leo aliipatia Azam penati mnamo dakika ya 58 ya mchezo iliyoingizwa kimiani na Aggrey Morris baada ya mchezaji wa wagosi Yusuph Chuma kucheza madhambi eneo la hatari.

Kutokana na matokeo hayo Coastal Union watakuwa na point 34 wakiendelea kujikita katika nafasi ya sita nyuma ya Mtibwa Sugar walio nafasi ya tano wakiwa na point 36 wakati huohuo timu ya wekundu wa msimbazi Simba wanashikilia nafasi ya nne wakiwa na point hizohizo 36 na Kagera Sugar yenye point 40 inashikilia nafasi ya tatu.

Hivyo ili Coastal Union wajiweke katika nafasi nzuri ni lazima washinde mechi zote mbili kati ya Yanga Mei 1 katika uwanja wa Taifa jijini na mechi dhidi ya Polisi Morogoro Mei 18 katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro. Kwani hizo point sita ukizidsha na point 34 itakuwa ni point 40 ambapo hata tukiwa nafasi ya nne si mbaya kikubwa ni kuwaombea mabaya Simba na Mtibwa Sugar katika mechi walizosalia nazo.

COASTAL UNION
costalunion@gmail.com
26 April, 2013
Dar es Salaam, Tanzania

Coastal Union kumenyana na Azam FC Mkwakwani leo.

Kocha mkuu wa Coastal Union akiwapa mawaidha wachezaji wake baada ya mazoezi. Hii ilikuwa ni Zanzibar, wakati wa kombe la mapinduzi.

Timu ya coastal Union kutoka Tanga leo itashuka dimbani kumenyana na Azam FC katika uwanja wa Mkwakwani Tanga.

Wagosi wa kaya ambao wanacheza mchezo huu ikiwa ni miongoni mwa michezo mitatu muhimu iliyobakia kwao kumaliza ligi kuu, kwa bahati mbaya wagosi hawatafuti chochote zaidi ya kulinda heshima yao na kubakia kwenye ligi kuu ili msimu ujao waweze kujipanga vema.

Mei 1, 2013 watacheza mechi yao ya pili dhidi ya Yanga katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ambapo mchezo huo utakuwa kama sikukuu kwa Yanga kwani wakishinda ama kutoa suluhu ya aina yoyote basi watafanikiwa kutangaza ubingwa kupitia mgongo wa Coastal Union ambapo itakuwa ni aibu kubwa kwa timu hiyo ya Tanga.

Mechi ya mwisho kwa wagosi itapigwa katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro Mei 18 dhidi ya maafande wa Polisi Morogoro ambao wapo katika hatihati ya kushuka daraja katika ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara.

Nafasi ya sita wanayoshikilia Coastal Union na point 33 si malengo ya timu hiyo iliyorudi kwa kasi katika ligi kuu ya Soka Tanzania bara, kwani walipanga msimu huu wamalize nafasi tatu za juu ili walau washiriki mechi za kimataifa zitakazowasaidia kujipima nguvu na timu nyingine barani Afrika.

Lakini malengo hayo yamekwenda harijojo baada ya kushindwa kuipigania nafasi ya tatu iliyokuwa imewachwa wazi na Simba zaidi ya mara tatu mpaka Kagera Sugar ilipoamua kuukata mzizi wa fitina na kujiweka katika nafasi ya tatu na kwa namna ligi inavyokwenda kuna hatihati Coastal Union ikashuka nafasi zaidi ikiwa watafanya uzembe kwa kutozichukua point 9 zilizobakia kwa mechi tatu zinazowakabili ambapo moja kati ya hizo wanacheza leo kwenye uwanja wa nyumbani.

kila lakheri Coastal Union, kila la kheri soka la Mkoa wa Tanga.

COASTAL UNION
costalunion@gmail.com
26 Aptil, 2013
Dar es Salaam, Tanzania

Tuesday, April 23, 2013

Mchezaji wa Coastal Union Ibrahim Twaha 'Messi' aitwa timu ya Young Taifa Stars.

 Ibrahim Twaha (kulia) alipokuwa uwanja wa Manungu wakati Coastal Union ikipambana na Mtibwa Sugar.

Aliyempa jina la Messi hajakosea, mtoto huyu ana uwezo mkubwa wa kuondoka na kijiji na katibu tarafa wake.


Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametangaza timu ya pili ya Taifa (Young Taifa Stars) atakayoitumia kuangalia wachezaji ambao baadaye anaweza kuwajumuisha kwenye timu ya wakubwa.

Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam jumanne Aprili 23, Kim amesema timu hiyo ni sehemu ya mpango wa maendeleo wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) uliozinduliwa Aprili 4 mwaka huu ukilenga kuendeleza wachezaji.

“Huu ni mpango wa kuendeleza vipaji Tanania na timu hii inajumuisha wachezaji ambao wamepita umri wa kuchezea timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) na wakubwa ambao hawajapata fursa ya kuingia Taifa Stars, lakini nitatumia Young Taifa Stars kuangalia uwezo wao.

“Timu hii ni kiungo kati ya vijana na wakubwa. Wengi wa wachezaji watakuwa vijana, lakini wakubwa wachache watapata fursa ya kuwemo ili kuangalia uwezo wao hata kama huko nyuma waliwahi kuchezea Taifa Stars. Lakini timu hii vilevile ni changamoto kwa wachezaji wa Taifa Stars kuwa wapo wanaosubiri wazembee ili wachukue nafasi zao,” amesema.

Young Taifa Stars yenye wachezaji 30 itakuwa na kambi ya siku tano jijini Dar es Salaam kuanzia Mei 2 hadi 6 mwaka huu.

Wachezaji walioitwa ni Aishi Manula (Azam), Hussein Shariff (Mtibwa Sugar) na Ali Mustapha (Yanga) ambao ni makipa. Mabeki ni Kessy Hassan (Mtibwa Sugar), Kennan Ngoma (Barnsley FC, Uingereza), Himid Mao (Azam), Ismail Gambo (Azam), David Mwantika (Azam), Miraji Adam (Simba), Mohamed Hussein (Kagera Sugar), Waziri Salum (Azam), Samih Nuhu (Azam) na Emily Mgeta (Simba).

Viungo ni Haruna Chanongo (Simba), Edward Christopher (Simba), Mudathiri Yahya (Azam), William Lucian (Simba), Jonas Mkude (Simba), Hassan Dilunga (Ruvu Shooting), Jimmy Shoji (JKT Ruvu), Abdallah Seseme (Simba), Ramadhan Singano (Simba), Farid Mussa (Azam) na Vicent Barnabas (Mtibwa Sugar).

Washambuliaji ni Hussein Javu (Mtibwa Sugar), Jerome Lambele (Ashanti United), Zahoro Pazi (JKT Ruvu), Twaha Hussein (Coastal Union), Abdallah Karihe (Azam) na Juma Luizio (Mtibwa Sugar).

Akizungumza na blog ya Coastal Union Ibrahim Twaha ‘Messi’ alisema anashukuru sana kuona juhudi zake zinatambuliwa na kocha Kim, kwani hakutegemea kabisa kuitwa katika kikosihicho cha wachezaji 30.

Kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa hatua niliyofikia, ni ndoto zangu za siku nyingi kucheza timu ya Taifa ya wakubwa, tayari nimeshachezea timu ya wadogo na sasa ni wakati wangu kuonyesha uwezo. Nitahakikisha nafanya vema na nitaingia rasmi timu ya wakubwa,” alisema Twaha.

Kutoka Coastal Union wawakilishi wa wachezaji chini ya umri wa miaka 20 walikuwa ni Ibrahim twaha na Ramadhan Shame ‘Batista’, lakini kwa bahati mbaya ‘Batista’ hajapata bahati ya kuingia kwenye kikosi hicho.

COASTAL UNION
APRILI 23, 2013
DAR ES SALAAM, TANZANIA
</

Mechi ya Coastal Union na Azam yarudishwa nyuma...



Shirikisho la soka Tanzania (TFF) limerudisha nyuma siku moja mechi kati ya Coastal Union na Azam iliyokuwa ichezwe jumamosi na sasa itachezwa ijumaa kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga.

Ofisa habari wa TFF, Boniface Wambura alisema awali mechi hiyo namba 168 ilikuwa ichezwe Aprili 27, lakini imerudishwa nyuma kwa siku moja ili kuipa nafasi Azam FC kujiandaa kwa mechi ya marudiano ya raundi ya pili ya kombe la shirikisho dhidi ya AS FAR Rabat ya Morocco itakayochezwa kati ya Mei 3, 4 au 5 nchini Morocco.

Katika mchezo huo wa ugenini Azam inahitaji ushindi wa aina yoyote au sare ya mabao kufuzu kwa hatua ya 16 bora katika michuano hiyo yenye heshima kubwa barani Afrika.

Katika hatua nyingine mechi ya pili ya Coastal Union itakayochezwa Mei 1, katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam dhidi ya Yanga, ndiwo mchezo utakaoamua hatma ya ubingwa wa Yanga kwa msimu huu baada ya kushinda mechi iliyopita dhidi ya JKT Ruvu na kujizolea point 56 hivyo kubakisha point moja tu kufikisha point 57 ambazo hakuna timu yoyote itakayoweza kufikisha point hizo.

Hivyo ili kulinda heshima ya timu kutogeuka daraja la kuwapa watu ubingwa lazima vijana wa Tanga kucheza mpira wa uhakika ili kuwanyamazisha Yanga kama walivyofanya Mgambo JKT kutoka Tanga wiki iliyopita uwanja wa Mwakwani.

Baada ya mchezo na Azam halafu Yanga, timu ya Coastal Union yenye point 33 katika nafasi ya sita itabakisha mchezo mmoja dhidi ya Polisi Morogoro utakaochezwa katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro mwezi wa tano.

COASTAL UNION
23 April, 2013

<

Thursday, April 18, 2013

Coastal Union kushuka dimbani kuumana na Azam FC Aprili 27 mwaa huu.



 Coastal Union itaikaribisha Azam kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga katika mechi itakayochezwa Aprili 27. Uwanja wa Taifa utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Simba na Polisi Morogoro itakayofanyika Aprili 28. mechi nyingine ya Coastal union tachezwa May 1, 2013 dhidi ya Yanga katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


Yanga ambayo inafukuzia kwa karibu taji la Ligi Kuu ya Vodacom itapambana na JKT Ruvu katika mechi pekee ya ligi hiyo wikiendi hii itakayofanyika Jumapili (Aprili 21 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mbali ya mechi hiyo, nyingine zitakazochezwa mwezi huu ni kati ya African Lyon na JKT Ruvu itakayofanyika Aprili 24 kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam wakati Aprili 25 ni kati ya Ruvu Shooting na Simba kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

coastal union
Dar es Salaam, Tanzania
18 april, 2013



Tuesday, April 16, 2013

Sare ya bila kufungana kati ya Coastal Union na JKT Ruvu imeumiza wengi uwanja wa Mkwakwani leo.



Coastal Union ya Tanga imeshindwa kuutumia vema uwanja wake wa nyumbani Mkwakwani baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana na maafande wa JKT Ruvu kwenye ligi kuu ya sika ya Vodacom Tanzania bara.
 kikosi kilichocheza mechi ya leo ni kama kifuatacho:
1. SHABAN KADO
2. HAMADI JUMA
3. OTHMAN MANI
4. MBWANA KIBACHA
5. PHILLIP MUGENZI
6. RAZAKH KHALFAN
7. JOSEPH MAHUNDI
8. MOHAMED SOUD
9. PIUS KISAMBALE
10. SULEIMAN KASSIM SELEMBE
11. ATUPELE GREEN

Wachezaji wa akiba ni:

12. RAJABU KAUMBU (GK)
13. ISMAIL SUMA
14. ABDUL BANDA
15. DANNY LIANGA
16. MOHAMED HASSAN
17. SHAONGWE 
18. ALLY UFUDU

Kwa matokeo ya leo Coastal Union watakuwa wamejikusanyia point moja na kuendelea kubaki nafasi ya sita wakiwa na point 33.

kushindwa kungaa kwenye mechi ya leo imekuwa pigo sana kwa wagosi wa kaya kwani matarajio ya kumaliza nafasi nne za juu yanazidi kufutika kwani Kagera Sugar wenye point 37 na kushikilia nafasi ya tatu, Simba wanaoshika nafasi ya nne na Mtibwa Sugar wanaoshika nafasi ya tano wapo vizuri kushinda mechi walizobakisha hivyo kuna matumaini madogo kuwashusha.

COASTAL UNION
costalunion@gmail.com
16 April, 2013
Dar es Salaam, Tanzania

Saturday, April 13, 2013

Matatizo ya kiufundi yakwamisha Super Week. Maana yake Coastal Union watacheza mechi yao bila kurushwa LIVE na SuperSport.

Mechi tano kati ya sita za Super Week za Ligi Kuu ya Vodacom zilizokuwa zioneshwe moja kwa moja (live) na Kituo cha televisheni cha SuperSport cha Afrika Kusini sasa hazitaoneshwa kutokana na matatizo ya kiufundi.

Kwa mujibu wa Mtayarishaji Mtendaji (Executive Producer) wa SuperSport Kanda ya Afrika, Max Tshunungwa ambaye yuko nchini, wameshindwa kuonesha mechi hizo kutokana na matatizo ya kiufundi katika magari yao ya kurushia matangazo (OB van) yanayohudumia Afrika Mashariki- Kenya, Tanzania na Uganda.

Mechi hizo ni kati ya Azam na African Lyon, Yanga na Oljoro JKT, Azam na Simba, Coastal Union na JKT Ruvu na Mgambo Shooting na Yanga itakayochezwa Aprili 17 mwaka huu jijini Tanga.
Tatizo hilo pia limeathiri mechi za Ligi Kuu ya Kenya (KPL) ambazo hazitaonekana wikiendi hii. SuperSport ndiyo yenye haki za matangazo ya televisheni kwa ligi hiyo ya Kenya.

Tshunungwa amekutana na Sekretarieti ya TFF na Kamati ya Ligi kuelezea tatizo hilo. SuperSport kwa kushirikiana na Kamati ya Ligi na TFF watapanga mechi nyingine za Super Week kabla ya ligi kumalizika msimu huu.

Pia TFF, Kamati ya Ligi na SuperSport walikuwa na mkutano mfupi wa waandishi wa habari wakati wa mapumziko kwenye mechi ya leo kati ya Yanga na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa.


Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
13 April, 2013

Monday, April 8, 2013

Mechi ya Coastal Union na JKT Ruvu kuonyeshwa Live Super Sports.


MECHI SITA KUONEKANA SUPERSPORT ‘LIVE’ SUPER WEEK
Kituo cha televisheni cha SuperSport cha Afrika Kusini kitaonesha moja kwa moja mechi sita za Ligi Kuu ya Vodacom katika Super Week kati ya Aprili 11 na Mei 18 mwaka huu.

Mechi hizo ni kati Azam na African Lyon itakayochezwa Aprili 11 mwaka huu badala ya Aprili 10 mwaka huu kwenye Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi, Dar es Salaam. Yanga na Oljoro JKT ambayo sasa itachezwa Aprili 13 mwaka huu badala ya Aprili 10 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Azam na Simba itakayochezwa Aprili 14 mwaka huu badala ya Aprili 13 mwaka huu Uwanja wa Taifa, na mechi kati ya Coastal Union na JKT Ruvu itakayochezwa Aprili 16 mwaka huu badala ya Aprili 10 mwaka huu.

Mechi nyingine ya Super Week itakayochezwa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga ni kati ya Mgambo Shooting na Yanga itakayofanyika Aprili 17 mwaka huu badala ya Aprili 13 mwaka huu.

Pia mechi nyingine itakayooneshwa live na SuperSport ni kati ya Yanga na Simba itakayofanyika Mei 18 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kutokana na mechi za Super Week, mechi kati ya Mtibwa Sugar na Oljoro JKT iliyokuwa ichezwe Aprili 13 mwaka huu sasa itachezwa Aprili 17 mwaka huu Uwanja wa Manungu, Turiani mkoani Morogoro.
 Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Aprili 8, 2013

Tuesday, April 2, 2013

TFF watambua mchango wa mchezaji wa zamani Coastalunion aliefariki juzi na kuzikwa jana Mkoani Tanga.


RAMBIRAMBI MSIBA WA BEHEWA SEMBWANA
Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha mchezaji wa zamani wa timu za Coastal Union, TPC na Taifa Stars, Behewa Ali Sembwana (72) kilichotokea jana usiku (Machi 31 mwaka huu) mkoani Tanga.

Msiba huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti Sembwana akiwa mchezaji, alitoa mchango mkubwa kwa timu mbalimbali alizochezea, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.

Sembwana aliyekuwa akicheza wingi ya kulia alidumu katika Taifa Stars kwa miaka kumi, kama ilivyokuwa kwa kombaini ya Mkoa wa Tanga (Tanga Stars) aliyoiwakilisha katika michuano ya Kombe la Taifa (Taifa Cup).

TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Sembwana, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Tanga (TRFA) na klabu ya Coastal Union na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.

Maziko yamefanyika jana (Aprili 1 mwaka huu) kijijini kwake Lusanga, Wilaya ya Muheza mkoani Tanga. Mungu aiweke roho ya marehemu Sembwana mahali pema peponi. Amina
COASTAL UNION
costalunion@gmail.com
Dar es Salaam, Tanzania
2 April, 2013