Tuesday, April 16, 2013

Sare ya bila kufungana kati ya Coastal Union na JKT Ruvu imeumiza wengi uwanja wa Mkwakwani leo.



Coastal Union ya Tanga imeshindwa kuutumia vema uwanja wake wa nyumbani Mkwakwani baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana na maafande wa JKT Ruvu kwenye ligi kuu ya sika ya Vodacom Tanzania bara.
 kikosi kilichocheza mechi ya leo ni kama kifuatacho:
1. SHABAN KADO
2. HAMADI JUMA
3. OTHMAN MANI
4. MBWANA KIBACHA
5. PHILLIP MUGENZI
6. RAZAKH KHALFAN
7. JOSEPH MAHUNDI
8. MOHAMED SOUD
9. PIUS KISAMBALE
10. SULEIMAN KASSIM SELEMBE
11. ATUPELE GREEN

Wachezaji wa akiba ni:

12. RAJABU KAUMBU (GK)
13. ISMAIL SUMA
14. ABDUL BANDA
15. DANNY LIANGA
16. MOHAMED HASSAN
17. SHAONGWE 
18. ALLY UFUDU

Kwa matokeo ya leo Coastal Union watakuwa wamejikusanyia point moja na kuendelea kubaki nafasi ya sita wakiwa na point 33.

kushindwa kungaa kwenye mechi ya leo imekuwa pigo sana kwa wagosi wa kaya kwani matarajio ya kumaliza nafasi nne za juu yanazidi kufutika kwani Kagera Sugar wenye point 37 na kushikilia nafasi ya tatu, Simba wanaoshika nafasi ya nne na Mtibwa Sugar wanaoshika nafasi ya tano wapo vizuri kushinda mechi walizobakisha hivyo kuna matumaini madogo kuwashusha.

COASTAL UNION
costalunion@gmail.com
16 April, 2013
Dar es Salaam, Tanzania

No comments:

Post a Comment