Sunday, March 31, 2013

Picha maalum...

Kocha wa timu B, Bakari Shime (kulia), na Meneja wa timu hiyo Ubinde (kushoto), wakiwa na Hafidh Kido mwandishi wa Coastal Union na mwendesha blog hii wakati wa chakula muda mfupi kabla ya mechi jana.

 Wachezaji wakishuka uwanjani kuingia vyumba vya kubadilisha nguo uwanja wa Azam Complex Chamazi uliozinduliwa rasmi na Rais Jakaya Kikwete wiki iliyopita.

Eddy na Ubinde wakizungumza na Philip Mugenzi beki wa kutumainiwa Coastal Union, Philip jana hakucheza kwani alikuwa na kadi tatu za njano hivyo nafasi yake ikachukuliwa na Yusuph Chuma kutoka timu B.

Hasira zimeshaniisha naendelea na picha mechi ya jana...

 Manahodha wa Lyon na Wagosi Obina Salamsasa na Mbwana Kibacha wakisalimiana na waamuzi kabla ya mechi.

 Benchi la wagosi wa kaya likiwa na tafakuri wakati kipyenga kinapulizwa kuashiria mchezo umeanza.

 Wanazi wa Coastal Union wakifuatilia kwa makini mchezo wa jana hapa kila mtu alikuwa na matumaini.

 Danny Lyanga aliniudhi sana jana, amekosa magoli mengi sana akiwa na golikipa tu, hapa akijilaumu.

Ohahaaa ohahaaa ehhaaa Doctor... au basi.. Daktari wa timu huyu Coastal Union siku za usoni nitawaletea historia yake hapahapa katika blog yetu. Alianza akiwa mchezaji wa Coastal Union, baada ya kuumia akashauriwa awe Daktari... yote hayo utayapata hapahapa. Kwa udhamini wa Binslum company Limited.

 Huyu Golikipa wa Lyon ni mzuri sana ila amejaa vituko ambavyo vitamsababishia kuharibu kipaji chake.

 Siku ya jana aliingia mpaka uwanjani na kumchezea madhambi Joseph Mahundi wa Coastal Union, hapa mwamuzi anataka kumpa kadi ya njano ndiyo anapiga magoti. Kumbe hiyo ilikuwa ni kadi yake ya tatu katika msimu hivyo atakosa mechi ijayo.

 Makamu Mweneyekiti wa Coastal Union Steven Mnguto akiingia uwanjani na mke wa mchezaji wa kibrazil Gabriel Barbosa. Kwa jaaam namuona Ally Mmahara au Kiraka mzee wa rally.


 Benchi la ufundi la African Lyon likiongozwa na kocha Charles Otieno wa kwanza kuanzia kushoto mwenye miwani meusi.

 Pius akiongoza kigoma uwanja wa Azam Complex Chamazi jana.

 Mwenyekiti Hemed Aurora, Meneja wa timu Akida na kocha wa timu B Bakari Shime wakiangalia vijana.

 Waanazi wa coastal Union wakiwa na matumaini makubwa ya ushindi wakati mchezo unaanza jana.

Eddy, Baba Willy (dereva wa Coastal Union katikati), na mzee Ally pembeni mshabiki mwingine wa Coastal Union wakifuatilia mchezo wa jana hapa ni baada ya kufungwa moja.

Saturday, March 30, 2013

Yaani leo sitaki kuzungumza kitu chochote, kufungwa 1-0 na African Lyon kumeninyima raha sana.

 Wachezaji wa coastal Union walikuwa wakiingia mpaka golini lakini hata sijui kwanini hawakutumia vema nafasi hizo.

 Selembe hapa akiwa ameweka gambani mpira ambao alitakuwa kumuachia Barbosa halafu yeye akatanua.

 Barbosa akitafuta mbinu za kumtoka beki wa African Lyon katika mechi ya leo uwanja wa Azam Complex.

 Amani Kyata wa African Lyon akimiliki mpira mbele ya Ibrahim Twaha na Danny Lyanga huku Abdi Banda akiwa tayari kutoa msaada.

 Mchezaji wa African Lyon Sunday Bakari akionyeshwa kadi ya njano na mwamuzi wa leo baada ya kumchezea madhambi Joseph Mahundi.

 Ibrahim Twaha 'Messi' akijaribu kushindana nguvu na mpira uliopigwa na Yusuph Chuma ingawa hakuupata.





 Kikosi cha Coastal Union kilichoanza leo dhidi ya African Lyon ambapo walilala 1-0.

 Kikosi cha African Lyon kilichokiadhiri kikosi cha wagosi wa Kaya leo.

Mpira ukionekana kukimbilia wavuni baada ya adhabu ndogo iliyopigwa na Gabriel Barbosa kipindi cha kwanza ingawa golikipa wa African Lyon Abdul Seif aliuwahi.

Mashabiki wa Coastal Union wakijadiliana cha kufanya baada ya kufungwa mchezo wa leo ambao ulikuwa ni muhimu kushinda.

COASTAL UNION
costalunion@gmail.com
30 March,2013

Tathmini mechi ya leo....


Mechi za leo ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara mzunguko wa pili ni Simba dhidi ya Toto African, Kagera Sugar dhidi ya Mtibwa sugar, Ruvu Shooting dhidi ya Azam FC, JKT Oljoro dhidi ya JKT Ruvu, Polisi Morogoro dhidi ya Yanga, na Coastal union dhidi ya African Lyon.


Kama tulivyotangulia kusema jana mechi ya leo ni ngumu na tunahitaji ushindi kwa hali na mali, kwasababu mahasimu wetu wote wanashuka dimbani leo, yaani Simba ambao wanacheza na Toto African mjini Mwanza, Kagera Sugar wanacheza na Mtibwa Sugar Bukoba uwanja wa Kaitaba.

Hivyo ili Coastal Union tukamate nafasi ya tatu ni lazima kushinda mechi ya leo hata kwa goli moja ili tupate point tatu muhimu zitakazotupatia point 37.

Hata hivyo lazima tuombe mabaya kwa Simba SC wafungwe au watoe suluhu mechi ya leo ili wabaki na point 34 hizohizo au 35. halafu Kagera Sugar wafungwe na Mtibwa Sugar wenye point 31 ama watoe suluhu ili wabaki na point 34 au 35.

Naam hili ni jambo la kawaida sana katika mchezo wa soka kuombeana mabaya, si dhambi bali ni kanuni za kisoka kukusanya point nyingi iwezekanavyo na kuomba mpinzani wako apoteze point nyingi iwezekanavyo.

Ligi bado ni ngumu kwani hata hao Yanga wanaotajwa kuwa mabingwa wakiwa na point 48 bado wana kazi ngumu ya kushinda mechi zote tano walizobakisha kwani hata Azam FC wenye point 40 wana nafasi kubwa ya kushinda mechi walizobakisha, ingawa Simba wanaojikongoja wameshapoteza matumaini ya kutetea ubingwa wao ndiyo maana tunaminyana nao katika nafasi ya tatu.

Mungu ibariki Tanga Mungu ibariki Coastal Union katika mchezo wa leo dhidi ya vibonde African Lyon uwanja wa Azam Complex Mbande jijini Dar es Salaam.

COASTAL UNION
30 March, 2013
Dar es Salaam, Tanzania



Thursday, March 28, 2013

Mechi ya kesho ushindi lazima. Nasikia harufu ya kombe la shirikisho...

 Wagosi wa kaya wlipokuwa uwanja wa Manungu wiki iliyopita Mkoani Morogoro kupambana na Mtibwa.

La Kapiteni Mbwana Kibacha akipeana mkono na Nahodha mwenzie wa Mtibwa Sugar kabla ya mchezo ulioshia kwa suluhu 1-1.


Timu ya Coastal Union kesho inashuka dimbani kumenyana na African Lyon kwenye uwanja wa Azam Complex Mbande jijini Dar es Salaam.

Wagosi wa kaya wanacheza mchezo wao wa 21 katika ligi ambao unakuwa ni mchezo wa tisa kwa mzunguko wa pili wa ligi hii ya Vodacom Tanzania Bara; ambapo kauli mbiu ya mechi ya kesho ni ushindi lazima kwani kwa kufanya hivyo itakwea mpaka nafasi ya tatu na kuwa na nafasi nzuri ya kubaki kwenye nafasi hiyo mpaka msimu unaisha ikawa watashinda mechi nne zilizobaki kukamilisha msimu wa 2012/2013.

African Lyon ambao wapo katika nafasi tatu za chini wapo katika hatihati ya kushuka daraja msimu huu hawatarajiwi kuleta madhara yoyote kwa wagosi ingawa mpira wa miguu hautabiriki wala haugangwi, hivyo matokeo yoyote yanaweza kutokea ikiwa wachezaji hawatotumia vema nafasi watakazopata kwani kwa mujibu wa kocha mkuu wa wagosi Hemed Morroco, wachezaji wapo fiti kwa mchezo.

Itakumbukwa huu ni mchezo wa tatu wenye ‘presha’ kwa vijana wa Tanga kwani mchezo wa kwanza ulikuwa ni dhidi ya wekundu wa Msimbazi Simba ambapo laiti wagosi wangeshinda mchezo ule basi wangeshika nafasi ya tatu, lakini kwa bahati mbaya wakapoteza mchezo ule kwa mabao 2-1.

Mchezo wa pili ulikuwa ni dhidi ya Mtibwa Sugar uwanja wa Manungu Turiani, ambapo wagosi wangeshinda mchezo ule wangekuwa na point 34 sawa na Simba lakini vijana wakaishia kutoa suluhu ya 1-1 hivyo kupata point 32.

Aidha kutokana na Simba SC kushindwa mchezo wa jumatano Machi 27 uwanja wa Kaitaba dhidi ya Kagera Sugar kwa bao 1-0, nafasi ya tatu inayoshikiliwa kwa muda na wekundu hao wa msimbazi wanaoandamwa na migogoro kwenye timu yao kiasi wachezaji na wapenzi kupoteza matumaini ya kutetea ubingwa wao, imekuwa wazi kwa timu tatu za Kagera Sugar wenye point 34, Mtibwa Sugar wenye point 32 na Coastal Union wenye point 32.

Hivyo lazima wachezaji wa Coastal Union kupitia nahodha wao Mbwana Kibacha, kutambua macho ya wakazi wa Tanga yote yapo miguuni mwao kuhakikisha heshima ya soka inarudi mkoani mwetu kwa kushinda mechi ya kesho tena kwa magoli mengi ili kuepuka kuandamwa na mahasimu wetu Simba SC, Mtibwa Sugar na Kagera Sugar wanaoonekana kuitaka kwa kasi zote nafasi hiyo.

COASTAL UNION
Dar es Salaam, Tanzania
29 March, 2013 

Kama wewe ni mpenzi wa kweli wa Coastal Union soma hii, na hakikisha imekubadili fikra.


Ndugu zangu,

Klabu yetu imeanza kurudi midomoni mwa wapenzi wa Soka si mkoa wa Tanga tu bali Tanzania nzima. Muda si mrefu ikiwa malengo yetu yatatimia, kumaliza ligi tukiwa nafasi tatu za juu tutaanza kujulikana Afrika.

Mara nyingi kitu kizuri hutengenezwa kwa juhudi za wachache waliojitolea kwa hali na mali kuhakikisha kitu hicho husimama tena kwa miguu miwili.

Hakuna kitu kibaya kama kuona nguvu, muda na mali ulizotumia kusimamisha kitu mpaka kikapata miguu kinaharibiwa kwa dhana tu.

Naam, dhana ya watu kutaka kuihujumu timu ya Coastal Union imejaa kwenye vichwa vya mashabiki wengi; watu hawakamatiki na hakuna anaempa muda mwenzake kuzungumza. Hujuma ndiyo mada kuu, makundi yametengenezwa kuhakikisha hujuma hizo zinasitishwa.

Cha kusikitisha, kila kundi linanyoosha kidole kwenye kundi jingine kuwa kundi lile linataka kuihujumu timu yetu iwe inafungwa. Ama kundi lile linataka kuchukua uongozi ili liongoze kwa namna wanayotaka wao, ama kundi lile linataka kubaki kwenye uongozi wa timu ili wale pesa.

Sidhani kuna mtu anaweza kupewa muda azungumzie dhana yake mbele ya umati wa wapenzi wa Coastal Union, na akazungumza kama anavyozungumza anapokuwa pembeni.

Hatuwezi kuishi kwa dhana, lazima tujiulize uongozi uliopo madarakani umetumia mbinu gani mpaka leo hii timu imekuwa miongoni mwa timu nne zinazotajwa kwenye vyombo vya habari kila uchao.

Pesa si kitu, lakini si kila mtu anaweza kutia mkono mfukoni mwake akaisaidia timu. Na mapenzi ya timu si kitu, lakini si kila mtu anaweza kuwa na mapenzi ya dhati kwa timu kuliko mwengine.

Wapo wanazi wa Coastal Union, ambao timu ikifungwa wanalia, lakini masikini ya Mungu hawana uwezo wa kuchangia hata nauli ya kumfikisha Mbeya kuitazama timu ikicheza na Tanzania Prisons.

Kila mtu ana haki ya kufikisha mawazo yake, ila njia zinazotumika kufikisha mawazo hayo zinatia ukakasi sana. Matusi, dharau, kedi na kunyoosheana vidole si njia bora za kukosoana.

Tunaona namna timu kubwa ambazo si ajabu nikizitaja hapa Yanga na Simba, timu inapokuwa na migogoro basi hata uwezo wa wachezaji unashuka. Hatutaki kufika huko, tuna msimu wa pili tu tangu timu irudi ligi kuu kwa kishindo. Kunazungumzwa maneno mengi sana, lakini hayaonyeshi njia za kutatua matatzo tuliyo nayo.

Huu si msimamo wa timu, lakini kama timu ya waandishi wa Coastal Union hili tatizo la maneno maneno kwenye timu linatupa wakati mgumu sana kujibu maswali magumu kutoka kwa wapinzani wetu huko mtaani.

Ipo haja uitwe mkutano wa wanachama ili kila mwanachama alie hai, namaanisha alielipia ada ya uanachama. Azungumze kinachomgusa katika timu na atoe dukuduku lake katika mkutano.

Angalizo:

Kinachofanyika kwenye kurasa za facebook si kitu chema, maana wanaingia watu wengi wazuri na wabaya.

Cha kushangaza kuna watu hawatumii majina yao ya asili bali wanazungumza maneno mabaya kuhusu viongozi wetu. Itafika wakati mtu ambae hatumii jina halisi atatolewa katika ukurasa wa timu ili kuepusha kuingiza mamluki ambao inawezekana wametumwa kuja kuivuruga timu yetu ya wastaarabu.

Tanga ni mji unaotajika kwa watu wenye hekima na busara, tungependa hekima na busara hizo zitumike katia kujadili mustakabali wa timu yetu.

Wakatabahu

COASTAL UNION
28 March, 2013  
<

Tuesday, March 26, 2013

Hizi ndizo mechi tano zilizobaki kukamilisha msimu.

Hii ndiyo ratiba ya mechi zilizobaki Coastal Union ligi kuu mzunguko wa pili. Tarehe 30 March tunacheza na African Lyon DSM. Tarehe 10 April, tunacheza na JKT Ruvu Tanga. Tarehe 27 April, tunacheza na Azam FC Tanga. Tarehe 1 May, tunacheza na Young African DSM. Na tarehe 18 May, tunacheza na Polisi Morogoro mjini Morogoro.

Coastal Union imebakisha mechi hizi ikiwa na point 32 nafasi ya nne, lakini ili kujihakikishia kubaki nafasi nne za juu ni lazima kushinda mechi zote ama kushinda mechi tatu muhimu za Azam FC kwakuwa inachezwa nyumbani, Arican lyon na vibonde wenzao wa Polisi Morogoro. JKT Ruvu wao ni wazuri, ila kwakuwa wanakuja nyumbani lazima watulizwe.

Yanga hata wao wanafungika ingawa wanacheza kwao, ila wana fitina nyingi sana za nje na ndani ya mchezo. Tukipata suluhu pia si mbaya lakini tunataka ushindi kutoka kwao. 

COASTAL UNION
DAR ES SALAAM, TANZANIA
26 MARCH, 2013

Thursday, March 21, 2013

Coastal Union, Milovan waanza mazungumzo



Jessca Nangawe 
Dar es Salaam. Uongozi wa klabu ya Coastal Union ya Tanga umeanza mazungumzo na aliyekuwa kocha wa Simba Curkovic Milovan kwa ajili ya kuifundisha timu hiyo msimu unaokuja wa Ligi Kuu. 

Kocha wa sasa, Hemed Morocco mkataba wake unatarajia kumalizika mwishoni mwa msimu, na kama watamalizana vizuri na Milovan basi huenda akawa kocha wao mpya mwakani. 

Afisa habari wa Coastal Union Edo Kumwembe alisema jana kuwa, tayari wamefanya mazungumzo na kocha huyo. 
Kumwembe alisema, mazungumzo ya awali yanaonyesha kuwa yuko tayari kujiunga na Union msimu ujao. 

Milovan alionyesha nia ya kuifundisha Coastal na sisi hatuna pingamizi naye kwani kocha wetu Morocco anamaliza mkataba wake mwishoni mwa msimu huu, alisema Kumwembe. 

Aliongeza:
Tunataka mazungumzo yetu yamalizike mapema ili kama kuanza kazi aanze mara tu msimu utakapomalizika. Tunamfahamu vyema Milovan ni kocha mzuri, atatufaa kuijenga timu yetu. 

Milovan ameifundisha Simba katika vipindi viwili tofauti, ambapo mara ya mwisho alitimuliwa mwishoni mwa mzunguko wa kwanza ligi.
Chanzo: Gazeti mwanaspoti.

Monday, March 18, 2013

Sakata la Nsa Job kusema amesuswa na Coastla Union laanza kupamba vyombo vya habari Tanzania.

 Nsa Job baada ya kuwekewa Plasta Of Paris (POP), tayari kwa safari kuelekea India kwa matibabu zaidi.

 Nsa Job akifanyiwa vipimo kuangalia athari ya goti lake la kushoto ili kuonenaka atatibiwa vipi.

 Nsa Job akiwa nchini India baada ya kufanyiwa Matibabu kwa saa nane mfululizo na hapo yupo fiti.

 Vyombo vya habari viliripoti kwa sana suala la Nsa job mshambuliaji hatari nchini kupelekwa India kwa gharama za timu.

Hii ni siku aliyoumizwa vibaya tarehe 28 October, 2012 uwanja wa Chamazi Coastal Union ilipocheza na JKT Ruvu mzunguko wa kwanza ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara. Saa hiyohiyo alipakiwa kwenye gari na kupelekwa hospitali kwa matibabu zaidi. Kabla ya kupelekwa India siku chache zilizofuata.

Hii picha ilipigwa saa chache kabla ya timu kuelekea uwanjani kupambana na Simba SC tarehe 10 March wiki iliyopita. Suala lililokuwa likizungumziwa hapa Meneja wa timu Akida alievaa nguo nyekundu, alimfikishia malalamiko mkurugenzi wa ufundi Nassor Mohammed 'Binslum' alievaa shati jeupe kuhusu mchezaji Nsa Job alieipa mgongo Camera. Arudi kambini mjini Tanga kwani anaonekana ameshakuwa fit.

Sasa tujadili pamoja, ikiwa timu imemsusa na haina haja nae Meneja Akida angekuwa na haja ya kumfikiria arudi kambini?


Coastal wakana kumtosa Nsa Job

NA SOMOE NG`ITU
18th March 2013
Uongozi wa timu ya Coastal Union ya jijini Tanga umekanusha taarifa za kumtelekeza mshambuliaji wake,Nsa Job na pia ikisema nyota huyo ana mkataba na klabu hiyo hadi Mei mwakani. Akizungumza na gazeti hili msemaji wa Coastal Union, Eddo Kumwembe, alisema kuwa wanasikitika kusikia taarifa za kumtelekeza Job wakati uongozi unampa huduma zote muhimu kama wachezaji wenzake wanavyopata licha ya kutocheza. 

Kumwembe alisema kuwa Job ambaye alipelekwa India na timu hiyo kwa ajili ya upasuaji, analipwa mishahara yake kila mwezi na pia motisha. 

Alisema pia mmoja wa viongozi wa timu aliyeko jijini Dar es Salaam, Nassor Binslum, amekuwa akimpa fedha kwa ajili ya kwenda hospitali kila anapohitaji kufanya hivyo.

''Ukweli ni kwamba uongozi wa Coastal unashangazwa sana na taarifa hizo ambazo kwa upande mmoja au mwingine inasemekana Nsa mwenyewe anachangia kuzisambaza,'' alisema Kumwembe. 

Aliongeza kwa kusema kwamba uongozi unamkaribisha mshambuliaji huyo kwa mazungumzo ya kuvunja mkataba wake kama anafikiria kufanya hivyo. Pia alimaliza kwa kuwataka wachezaji wa Coastal wenye mikataba  kutozungumza na vyombo vya habari bila ya ruhusa ya klabu. Nsa hakupatikana kuzungumzia suala hilo 
 
CHANZO: NIPASHE

Habari picha kutoka Manungu juzi.....

 Mwalimu Hemed Morroco anapenda sana mpira wa darasani, akiingia uwanjani ana kauli moja 'mchezaji cheza kama nilivyokufundisha halafu onyesha uwezo binafsi'.

 Admin wetu alichelewa kufika Turiani, alifika dakika chache kabla ya timu kuondoka kambini kuelekea uwanjani.

 Vijana wakipasha kuondoa uchovu wa safar na ushinda hofu, maana mechi ilikuwa ngumu kama fainali.

 Ally Mohammed 'Kidi' kocha msaidizi wa Coastal Union mwenyewe anasema 'mie Polisi sizungumzi sana vtendo tu'.

 Shaaban Kado alikuwa na wakati mgumu sana kushndana na mashabiki wake wa zamani, kwani walikuwa wakimzomea uwanjani ati ni msaliti kwa kuiwacha Mtibwa Sugar na kukimbilia Coastal Union. Ila kama kawaida yake uzoefu ulimsaidia sana.

 Kit Manager Mohammed, juzi alikuwa na furaha maana ana moyo mlaini sana. Timu ikifungwa analia. mahaba mabaya.

 Kocha Mecky Mexime wa Mtibwa Sugar wa kwanza kulia akiwatazama vijana wake, huyu ni mnazi wa Mtibwa mbali ya kuwa mwajiriwa lakini Mtibwa ndiyo iliyomlea hata akawa nahodha wa Taifa Stars kwa kipindi kirefu.

 Meneja wa timu Akida, akiwatazama vijana wake wakipata kumbukumbu ya Turiani Madizini.

Raha ya Mpira ni kujua kuwa soka ni burudani, manahodha wa timu zote wakipeana mikono kuashiria 'Fair Play'.

Sunday, March 17, 2013

Jana mpira ulichezwa uwanjani huku nje ya uwanja mashabiki waliotoka Tanga wakivamia ngoma za watu...

 Watu wanacheza mpira huku kigoma cha Coastal Union kimevamia kigoma cha Mtibwa Sugar, Pius yu teleeeee hapa.

 Rajab Mohammed akimiliki mpira huku Ibrahim Twaha akitafuta mbinu za kuuiba akimbie nao.

 Gabriel Barbosa akijitahidi kukimbia kwa nguvu zake zote kuuwahi mpira uliopigwa na Danny Lyanga (hayupo pichani).

                                                     AAahhhhhhh Baba Nzori weeeee.....

 Wadau wa Coastal Union wakiangalia kwa makini mchezo wa jana, watu wana moyo na timu balaa.

 Jamani mtaona kama huyu mtoto nampendelea lakini ilikuwa kila nikiinua Camera basi lazima amekaa mkao mzuri wa kupigwa picha. Waandishi wanapenda picha zinazozungumza.... Mtanisamehe...


 Beki wa Coastal Union Phili Mugenzi akilalamika baada ya pasi aliyodhamiria kumpa Gabriel Barbosa kudakwa na mchezaji wa Mtibwa.

 Abdi Banda alieingia kipindi cha pili akipga kona ambayo hata hivyo haikuzaa matunda. Unajua nini, alinambia nimpige picha kisa amevaa mnyama (kiatu) mpya.

Danny Lyanga akikokota mpira pembezoni mw uwanja huku beki wa Mtibwa akiwa tayari kuzuia madhara yoyote yatakayosababishwa na Danny.

Makocha wa timu zote mbili wakipongezana kwa suluhu ya 1-1 baada ya dakika tisini za mchezo kuisha.