Thursday, February 27, 2014

Coastal Union waitwa wawili Taifa Stars.

Abdi Banda
                                                             Shaaban Kado

Kutokana na mechi dhidi ya kirafiki dhidi ya Namibia itakayochezwa Machi 5 mwaka huu jijini Windhoek, Stars itaongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Ufundi, Salum Madadi akisaidiwa na kocha Hafidh Badru kutoka Zanzibar.

Katika hatua nyingine, Kocha Madadi amewaondoa wachezaji watano wa Yanga katika kikosi kilichotajwa awali ili wapate fursa ya kuitumikia timu yao kwenye mechi mbili za Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al-Ahly ya Misri.

Wachezaji hao ni Athuman Idd, David Luhende, Deogratius Munishi, Frank Domayo, Kelvin Yondani na Mrisho Ngasa. Pia kipa Ivo Mapunda ameondolewa katika kikosi hicho baada ya kupata msiba.

Nafasi zao zimezibwa na wachezaji Abdi Banda (Coastal Union), Himid Mao (Azam), Juma Luizio (Mtibwa Sugar), Said Moradi (Azam) na Shabani Kado (Coastal Union).

Taifa Stars itaingia kambini keshokutwa (Machi 1 mwaka huu) jioni kwenye hoteli ya Accomondia jijini Dar es Salaam, na itaondoka Machi 3 mwaka huu alfajiri kwa ndege ya South African Airways na kurejea nchini Machi 7 mwaka huu saa 8.15 mchana.
HAFIDH KIDO
MSEMAJI COASTAL UNION
28 FEB, 2014


Tuesday, February 25, 2014

Bakari Jeki kuzikwa leo Muheza.



Bakari Jeki wa kwanza kulia alievaa kofia akiwa na mbunge wa Tanga, Omar Nundu enzi za uhai wake.

KWA niaba ya uongozi wa Coastal Union, tunatangaza msiba wa mchezaji wa zamani wa timu hii Bakari Jeki, aliefariki usiku wa kuamkia jana katika hospitali ya rufaa Bombo.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa kaka wa marehemu ndugu Ally Jeki, ndugu yetu aliugua kwa muda mfupi ambapo alilazwa katika hospitali ya Bombo wiki iliyopita mpaka mauti yalipomfika siku tatu baada ya kuanza kuugua.
Mwandisi wetu alizungumza na mchezaji wa zamani wa Coastal Union, ambae alipata bahati kumuona Bakari Jeki akiitumikia Coastal Union, Razak Yusuf ‘Careca’ ambae alibainisha kuwa marehemu alikuwa na mchango mkubwa katika timu.  
“Coastal Union imekosa mtu muhimu katika soka ambae alikuwa msaada mkubwa akitoa mawazo, vilevile alikuwa hakosi katika mechi na mazoezi ya timu,” Careca.
Aidha beki namba tano wa zamani Coastal Union, Mzee Salim Amir ambae alicheza na marehemu katika michuano ya UFUMA, iliyoandaliwa na Chama Cha Soka nchini (FAT), ambao ulikuwa ni ushauri wa Rais wa kwanza wa Tanzania, Julius Nyerere.
Nyerere alitoa ushauri huo ili kuisaidia FAT iliyokuwa chini ya Said El Maamry, kuondokana na madeni. Michuano hiyo ikapewa jina la Operesheni Futa Madeni (OFUMA).
Ilishirikisha timu nne ambazo ni Simba (Dar es Salaam), Nyota (Mtwara), Coastal Union (Tanga) na Nyota Afrika (Morogoro), Coastal Union waliibuka mabingwa marehemu Bakari Jeki akiwa beki mbili na langoni alikuwa mdogo wake Said Jeki ambae pia alikuwa golikipa wa Taifa Stars.
Baadhi ya wachezaji waliokuwa katika kikosi kilichotwaa kombe la OFUMA, ambalo lilichezwa mara moja tu na kutoendelea tena ni Zacharia Kinanda, Mohammed Makunda, Bakari Rashid, Kuzu Mbwana, Salim Amir, Mohammed Salim, Zaharan Makame, Said Jeki  na Mguruko.
“Alikuwa ni beki mzuri, Coastal Union ilinufaika na uchezaji wake kwani alicheza kwa moyo wote beki mbili ambayo ilipanda na kushuka bila kuchoka. Mbali na hayo aliishi vizuri na wenzake hakuwa mtu wa matatizo muda mwingi alipenda utani.
“Alinikuta mwaka1976 nikitokea Misri na timu ya Taifa, tukashiriki kombe la OFUMA tukiwa pamoja katika safu ya ulinzi lakini baadae nilistaafu baada ya kuumia, yeye aliendelea mpaka mwanzoni mwa miaka ya 1980 ndipo akaachana na soka, lakini hakuacha kuwa karibu na Coastal Union, muda mwingi alijitokeza kutoa ushauri na kila alipohitajika hakusita kuitikia mwito, huyo ndie Bakari Jeki ninaemfahamu,” alisema Salim Amiri.
Marehemu, alianza kucheza Coastal Union mwaka 1976 akitokea timu ya Magunia Moshi, alipotua Coastal Union alicheza kwa moyo wake wote mpaka alipostaafu soka, mpaka mauti yanamfika alikuwa kocha wa timu za mchangani mjini tanga na mshauri mkubwa wa benchi la ufundi Coastal Union.
Vilevile marehemu alitoka katika familia yenye vipaji vya soka kwani walikuwa ndugu watatu wa baba mmoja na mama mmoja ambapo Said Jeki alikuwa golikipa wa Coastal Union na timu ya Taifa, mwingine ni Hassan Jeki ambae alikuwa akichezea Reli Morogoro, lakini kwa sasa wote watatu ni marehemu.
Mwili wa Marehemu utatolewa Hospitali ya Rufaa Bombo mjini Tanga kuelekea nyumbani kwa kaka yake Ally Jeki maeneo ya Majengo, ifikapo saa tisa alasiri mwili wa marehemu utasaliwa katika msikiti wa Majengo kabla ya kupelekwa kijijini kwa Masuguru Wilayani Muheza Mkoani Tanga saa kumi alasiri.
Kaka wa marehemu hakuweka wazi kuhusu familia ya marehemu hasa uppande wa mke ama watoto lakini alibainisha kuwa marehemu alizaliwa mwaka 1953 wilayani Muheza, Tanga.
HAFIDH KIDO- MSEMAJI
COASTAL UNION
26 FEB, 2014


Sunday, February 23, 2014

Mechi saba za Coastal Union zilizobaki.



Ikiwa hakutakuwa na mabadiliko yoyote kutoka Shirikisho la soka nchini (TFF), mechi saba za Coastal Union zilizobaki msimu huu zitakuwa ni dhidi ya Ashanti United Machi 8, 2014 uwanja wa Mkwakwani Ifikapo Machi 12 katika uwanja wa Taifa jiji Dar es Salaam Wagosi  wa Kaya watacheza na Simba, wakati Machi 15 katika uwanja wa Azam Complex Chamazi, Wagosi watakipiga na Azam FC katika mechi ya 22 ligi kuu ya Vodacom.
Aidha ifikapo Machi 23 mwaka huu Wagosi wa Kaya watasafiri mpaka Manungu kumenyana na Mtibwa Sugar, na Machi 30 Coastal Union itafunga mwezi dhidi ya Mgambo JKT katika uwanja wa Mkwakwani Tanga huku Wagosi wakiwa wageni wa Mgambo.
Ifikapo Aprili 14, 2014 Coastal Union itakutana na JKT Ruvu katika uwanja wa Mkwakwani huku ikikamilisha ratiba ya Ligi kwa mechi dhidi ya Kagera Sugar katika uwanja wa Mkwakwani tarehe 27 April, mwaka huu.
Mpaka sasa Coastal Union imecheza mechi 19 tangu ligi ianze, imeambulia point 25 katika nafasi ya sita nyuma ya Yanga point 38, Azam (36), Mbeya City (35), Simba (32) na Kagera Sugar (26).
MSEMAJI- COATAL UNION
TANGA, TANZANIA
FEB 23, 2014

Coastal Union nafasi ya 6 point 25.

Rank
Teams
Played Wins Draw Lost GD Goal score Points
1 Yanga SC 17 11 5 1 29 41 38
2 Azam FC 16 10 6 0 19 29 36
3 Mbeya City 19 9 8 2 8 24 35
4 Simba SC 19 8 8 3 16 35 32
5 Kagera Sugar 19 6 8 5 1 17 26
6 Coastal Union 19 5 10 4 5 14 25
7 Ruvu Shooting 18 6 7 5 -4 19 25
8 Mtibwa Sugar 19 6 7 6 0 23 25
9 JKT Ruvu 19 7 1 11 -13 16 22
10 Mgambo Shooting 19 4 5 10 -17 11 17
11 Prisons FC 16 3 7 6 -3 13 16
12 Ashanti UTD 18 3 5 10 -15 15 14
13 JKT Oljoro 19 2 8 9 -15 14 14
14 Rhino Rangers 19 2 7 10 -11 12 13

Saturday, February 22, 2014

Coastal Union 2-0 Mbeya City

 Mashabiki wa Coastal Union wakishangilia baada ya kuingia bao la pili dakika chache kabla ya mpira kuisha.

 Kiungo mshambuliaji wa Coastal Union, Mkongwe Haruna Moshi Boba akitafuta mbinu za kumtoka nahodha wa Mbeya City katika mchezo wa leo.

 Ally Nassor 'Ufudu' akitumia mbinu za kumkinga golikipa wa Mbeya City katika moja ya kona zilizopigwa kwenye mchezo wa leo ulioisha kwa mshindi mnono wa bao 2-0.

Danny Lyanga akikokota mpira huku mchezai wa Mbeya City akitafuta mbinu za kumdhibiti.

 Yusuf Chipo akiwahimiza wachezaji wake wapande juu wasikabe.


Haruna Moshi 'Boban', akifanya vitu vyake uwanjani leo kuwaonyesha vijana kwamba bado yumo.

 Winga wa Coastal Union Danny Lyanga akiambaa na mpira huku akitafuta mbinu za kupiga krosi.

                                                                Danny Lyanga akiminyana.
 Mlinzi wa pembeni Coastal Union, Abdi Banda akimiliki mpira bila ya wasiwasi wowote.

Mohammed Miraji 'aliebebwa' akishangilia bao la kwanza mnamo dakika ya 79 kipindi cha pili.

mlinda mlango wa Costal Union Shaaban Kado, alishindwa kujizuia nae alikuja kushangilia bao la kwanza.


 Mashabiki wa Mbeya City wakiwa hawaamini wanachokiona namna vijana wa Chipo walivyofanya mambo.


 Mashabiki wa Caostal Union katika furaha kwenye uwanja wa nyumbani Mkwakwani.

                                                                Shaaban Kado.

 Kutoka kushoto Juma Nyoso, Mohammed Miraji na Kenneth masumbuko wakishangilia bao la pili lililofungwa na Moammed Miraji.

Mohammed Miraji akilia kwa uchungu baada ya kuweka historia ya kuwapiga mabao mawili peke yake Mbeya City.

 Mbeya City kawaida yao hufanya mazoezi baada ya mechi, lakini Mkwakwani walifanya kidogo na kuacha.


                                    Mashabiki wa Coastal Union wakishangilia baada ya mechi.

HATIMAE historia imeandikwa kwatika jiji la Tanga baada ya Coastal Union ‘Wagosi wa kaya’ kuwa timu ya pili kuifunga Mbeya City katika Ligi Kuu, lakini vilevile ni ya kwanza kuifunga mabao mengi.
Bao la kwanza liliingizwa kimiani mnamo dakika ya 79 baada ya Mohammed Miraji, kuunganisha pasi ya Danny Lyanga ambae alipokea mpira uliorushwa na Abdi Banda.
Mohammed, aliruka juu na mchezaji wa Mbeya City akapiga kichwa kilichopaa na kurudi langoni kama masihara ukisindikizwa na beki wa Mbeya City. Baada ya bao hilo Coastal Union waliendelea kulisakama lango la Mbeya City kwa takriban dakika tano.
Aidha bao la pili lilikuwa juhudi binafsi za mchezaji chipukizi Mohammed Miraji ‘Muddy Magoli’ ambapo alipokea pasi nyuma kidogo ya 18, akamzidi nguvu kiungo wa Mbeya City akapiga chenga mbili na kuinua macho kumtazama Burhani, golikipa wa Mbeya City. Akakunjuka shuti kali kwa mguu wa kulia lililomzidi nguvu Burhani na kuandika bao la pili dakika mbili kabla ya mwamuzi wa leo Zacharia Jacob, kutoka Pwani kumaliza mchezo.
Hata hivyo Wagosi wa Kaya walinza mpira wa leo kwa kusuasua ambapo kipindi cha kwanza walitengeneza nafasi nyingi lakini hawakuambulia kitu. Mpaka kipindi cha kwanza kinakamilika Wagosi walicheza chini ya kiwango hali iliyowanyima raha mashabiki wa Wagosi huku ikiwaamsha mashabiki wachache wa Mbeya City waliosafiri na timu kutoka jijini Mbeya.
Kocha wa Wagosi Yusuf Chipo, alifanya mabadiliko kwa kuwatoa Ally Nassor ‘Ufudu’ akaingia Kenneth masumbuko, baadae akamtoa Ayoub Semstawa akaingia Yayo kato halafu akakamilisha mabadiliko ya leo kwa kumtoa Crispian Odula na kumuingiza Mohammed Miraji ambae alikuwa mfalme wa echi ya leo.
Mabadiliko hayo yalileta uhai kwa timu hasa winga Masumbuko alipoingiza mipira mingi lakini Yayo kato na Haruna Moshi ‘Boban’ walishindwa kuzitendea haki krosi za winga huyo msumbufu.
Katika hatua nyingine Mbeya City, walifanya mashambulizi mengi katika lango la Wagosi lakini uimara wa mabeki Abdi banda, Nyoso, Kibacha na Chuma ulimsaidia golikipa Shaaban Kado kupata muda mzuri wa kudaka kwa kujiamini.
Kutokana na matokeo hayo Coastal Union wamepaa mpaka nafasi ya sita wakitoka nafasi ya saba huku wakijizolea point 25.
Kikosi cha leo: Shaaban Kado, Mbwana Kibacha, Abdi Banda, Yusuf Chuma, Juma Nyoso, Jery Santo, Dany Lyanga, Ally Nassor ‘Ufudu’, Ayoub Semtawa, Haruna Moshi ‘Boban’ na Crispian Odula.
Wachezaji wa akiba walikuwa ni: Mansour Alawi, Suleiman Kassim ‘Selembe’, Kenneth Masumbuko, Mohammed Miraji, Yayo kato, Behewa Sembwana na Ayoub Masoud.
COASTAL UNION
22 FEBRUARI, 2014
TANGA, TANZANIA

Coastal Union Vs Mbeya City

 Dany, Selembe na Santo wakimsikiliza mwalimu kwa umakini leo asubuhi katika kambi ya Coastal Union.

                                Kocha Yusuf Chipo akisisitiza jambo kabla ya mechi leo asubuhi.

                      Mtu mzima Boban, akitafakari namna atakavyowanyamazisha Wanyakyusa.


                                  " Lazima mucheze kwa kujiamini tupo nyumbani baanaaa.."

Kocha wa magolikipa Adam Meja na kocha msaidizi Ally jangalu wakifuatilia darasa la Mwalimu Chipo.



KOCHA wa Coastal Union, Yusuf Chipo amesema mechi ya leo ni ngumu haina matokeo lakini watakaoleta matokeo ni wachezaji baada ya kuamua kucheza kwa kujituma.
Chipo, ameongeza kuwa amesikia Mbeya City ni timu ngumu, lakini yeye hajui hilo kwasababu alipokuwa darasani akifundishwa ukocha ncini ujerumani, aliambiwa timu zote zinakuwa na wachezaji kumi ndani na golikipa mmoja.
“Sitegemei kuona kitu kipya kutoka kwa Mbeya City, bali nataka kuwaona nyinyi mnacheza kitimu na kujituma, sitaki mtu akae nyuma pelekeni timu mbele sisi tupo nyumbani tunataka ushindi. Kinachowasaidia Mbeya City kupata sifa ni kujituma, na hicho naamini hata nyinyi mnaweza,” alisema.
Baada ya hapo alitaja kikosi cha leo na kuwaambia macho ya mashabiki wa Coastal Union, kwenye mchezo huu wa Ligi Kuu Tanzania bara yapo miguuni mwenu, mkifanya vizuri ama mkifanya vibaya ni kwa mustakabali wa maisha yenu kisoka.
Kikosi cha leo kitakachoanza: Shaaban Kado, Mbwana Kibacha, Abdi Banda, Yusuf Chuma, Juma Nyoso, Jery Santo, Danny Lyanga, Ally Nassor ‘Ufudu’, Ayoub Semtawa, Crispian Odula na Haruna Moshi ‘Boban’.
Wachezaji wa akiba: Mansour Alawi, Suleiman Kassim ‘Selembe’, Yayo kato, Mohammed Miraji, Ayoub Masoud, Behewa Sembwana na Kenneth Masumbuko.
Coastal Union inashuka dimbani kumenyana na Mbeya City, wakiwa na point 22 nafasi ya saba katika msimamo wa ligi, ushindi wa leo dhidi ya Mbeya City utamaanisha vitu viwili, kupata uhakika wa kumaliza ligi nafasi nzuri na kuweka heshima kwa kuwafunga Mbeya City wanaotajwa kuwa wagumu kufungika.
HAFIDH KIDO
MSEMAJI CUSC
TANGA- TANZANIA
FEB 22, 2014