Thursday, July 23, 2015

COASTAL YAMNASA KIPA KUTOKA VILLA SC YA UGANDA”



 UONGOZI wa Klabu ya Coastal Union umeingia mkataba wa miaka miwili na aliyekuwa mlinda mlango wa timu ya Villa SC ya nchini Uganda, Jackson Sabweto ili kuitumikia timu hiyo katika msimu mpya wa Ligi kuu soka Tanzania bara utakaoanza mwezi Septemba mwaka huu.

Utiliaji saini huo ulifanyika juzi makao makuu ya klabu hiyo yaliyopo barabara kumi na moja jijini Tanga na kushuhudiwa na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu, Kassim El Siagi.

Akizungumza , Katibu wa Coastal Union, Kassim El Siagi alisema kuwa nia ya kumsajili kipa huyo ni kuimarisha nafasi hiyo kwenye timu hiyo kabla ya kuanza michuano ya Ligi kuu soka Tanzania ili waweze kushiriki kwa mafanikio makubwa na tija.

El Siagi alisema kuwa usajili ambao umefanywa na klabu umepanga kuhakikisha msimu ujao kombe la Ligi kuu linatua kwenye viunga vya mitaa ya barabara ya kumi na moja jijini Tanga ili kurudisha historia yao ya muda mrefu tokea walipotwaa kombe hilo mwaka 1988.

   “Niseme tu usajili tulioufanya ni nzuri na utakuwa chachu ya kurejesha makali yetu ya mwaka 1988 wakati tulipochukua Ubingwa wa Ligi kuu hapa nchini “Alisema El Siagi.

Hata hivyo aliwataka wachezaji ambao hawajawasili mkoani hapa kuungana na wenzao kwenye mazoezi yanayoendelea kwenye viwanja vya shule ya sekondari Popatlaly chini ya Kocha Mkuu, Jackson Mayanja kuhakikisha wanawasili haraka iwezekanavyo.

No comments:

Post a Comment