Monday, July 27, 2015

MWENYEKITI WA COASTAL UNION AKUTANA NA KAMATI MBALIMBALI

MWENYEKITI WA COASTAL UNION,DR.AHMED TWAHA AKIZUNGUMZA NA KAMATI ZA KLABU HIYO MWISHONI MWA WIKI KULIA NI KATIBU MKUU KASSIM EL SIAGI NA KUSHOTO NI MAKAMU MWENYEKITI SALIM AMII

MWENYEKITI WA COASTAL UNION DR.AHMED TWAHA AKIONGEZA MPANGO MKAKATI WA KLABU HIYO UTAKAOTUMIKA KATIKA KIPINDI CHA UONGOZI WAKE




MENEJA WA KLABU YA COASTAL UNION,AKIDA MACHAI AKISISITIZA JAMBO KWENYE MKUTANO HUO AMBAO ULIMUISHA KAMATI ZOTE ZILIZOUNDWA NA MWENYEKITI HUYO
WAJUMBE WA KAMATI MBALIMBALI WAKIMSIKILIZA MWENYEKITI WA COASTAL UNION,DR.AHMED TWAHA WAKATI WA KIKAO HICHO

\PICHA YA PAMOJA MWENYEKITI WA COASTAL UNION NA WAJUMBE WA KAMATI MBALIMBALI


     MWENYEKITI WA KLABU YA COASTAL UNION,DR.AHMED TWAHA AKIWA KWENYE PICHA YA PAMOJA NA KAMATI YA MIPANGO NA FEDHA.



UONGOZI wa Klabu ya Coastal Union umeitaka kamati ya ulinzi na usalama kuhakikisha inatimiza wajibu wake ipasavyo ikiwemo kuhakikisha vitendo vitakavyoweza kuigharimu timu hiyo wakati wa michuano ya Ligi kuu soka Tanzania bara vinazibitiwa.


Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa kikao baina ya Kamati ndogo ndogo zilizoundwa,Mwenyekiti wa Klabu ya Coastal Union,Dr.Ahmed Twaha alisema kuwa kumekuwa na vitendo vingi ambavyo vinajitokeza kwenye michuano ya Ligi kuu Tanzania bara na kuigharimu timu yetu na kulazimika kulipa faini ambayo ingeweza kufanya mambo mengine ya maendeleo.
Alisema kutokana na kuwepo kwa tatizo hilo ndio sababu pekee iliyopelekea kuundwa kamati hiyo ili kuweza kukabiliana na vitendo vinayoweza kuisababisha hasara ndani ya klabu hiyo kwani vinakwamisha juhudi za kupiga maendeleo.
   “Ukiangalia msimu uliopita tulipata hasara ya shilingi milioni 3 kwa makosa ya uwanjani na hii inasababishwa na mashabiki kitendo ambacho kinaharibu sura ya mkoa hivyo lazima kamati hii italisimamia suala hilo “Alisema Mwenyekiti huyo.
Aidha Mwenyekiti huyo aliitwisha mzigo mengine kamati ya Nidhamu na Maadili kuhakikisha watu wanaotukana kwenye mitandaa ya kijamii ikiwemo Facebook, Twiter na mengineyo watachukuliwa hatua kali za kisheria ili kukomesha vitendo hivyo.
Hata hivyo alisema kuwa kamati hiyo itakuwa na jukumu kubwa la kuhakikisha ulinzi na usalama unaimarishwa wakati wa timu hiyo itakapokuwa ikicheza mechi zake kwenye michuano ya Ligi kuu soka Tanzania bara.
 “Lakini pia zamani wapo watu walikuwa wakitengeneza vitabu vya tiketi na kufanya mapato kuwa madogo licha ya uwepo wa watu wengi hivyo huu ndio mwisho wao kamati hii pia itasimamia suala hilo kwani hali hii iliifanya klabu kukosa mapato “Alisema Mwenyekiti huyo.
Mwenyekiti huyo alisema kuwa wameweka mipango mizuri ya kuhakikisha timu hiyo inafungua matawi kwenye mikoa yote timu hiyo itakapokuwa ikienda kushiriki michuano ya Ligi kuu hapa nchini.

No comments:

Post a Comment