Tuesday, September 10, 2013

Coastal Union ya miaka ya nyuma imerudi tena... Kikosi cha ushindani.

 Kikosi cha zamani cha Coastal Union, Kuanzia kushoto wa kwanza ni Ali Mwaliza nyuma yake ni Yassin Napili, wa Kati ni Mohammed Kampira, Ally Maumba, Aggrey Chambo na Kassa Mussa, na wa kwanza ni Ali Majeshi wa nyuma ni Said Kolongo! Kikosi hiki ni baada ya ubingwa wa 1988.

                                                                     Ally Maumba. 

Umepita muda mrefu bila kupata taarifa za timu, lakini ni kutokana na kusimama kwa ligi kupisha mechi ya kumaliza kufuzu kwa michuano ya kombe la dunia, ambapo Taifa Stars imemaliza vibaya kwa kuchapwa na Gambia mabao 2 kwa 0.

Ligi itaendelea tena jumamosi Septemba 14 katika uwanja wa Mkwakwani ambapo Wagosi wa Kaya watakutana na maafande wa Prison kutoka Mbeya.

Itakumbukwa mechi mbili za awali Coastal Union ilishinda mabao 2 kwa 0 dhidi ya JKT Oljoro ya Arusha katika uwanja wa kumbkumbu ya Sheikh Amri Abeid, na kutoa suluhu ya 1 kwa 1 dhidi ya Yanga jijini Dar es Salaam katika uwanja wa Taifa.

Baada ya hapo jumapili Septemba 8, timu ilicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Mafunzo kutoka Zanzibar ambao nao ni askari magereza kama Prison, matokeo ilikuwa ni Coastal Union 1 na Mafunzo 0. Mfungaji akiwa ni mchezaji kutoka Uganda, Kato Yayo Lutimba.

Leo tunaendelea na kumbukumbu za wachezaji walioiletea mafanikio Coastal, ambapo jina la Ally Maumba ndilo linalopamba ukurasa wetu kwa leo, habari hii ilitolewa kwenye ukurasa wa facebook lakini wachangiaji ndiwo watakaoandika habari ya leo. Naleta maneno yao kama walivyoaandika kumzungumzia Legend huyu.

Dhulfikar Ashraf dogo alikua na uwezo wa ajabu lakini ni Coastal yote ilikua na uwezo kwakila mchezaji ukiacha Maumba Iddrisa Ngulungu naye alikua muhimu sana anajua kukaba kutoa pasi za mwisho alikua fundi sana kama Kasa Mussa, Juma Mgunda, Aly Ruga, Kasim Mwajek, Mohammed Kampira, Doglas Muhani, Abuu Napili, Joseph Lazaro, Razak Yussuph ‘Careca’ Agrey Chambo, Abubakari Hassani, Mohammed Mwameja,  Makena, Rifat Said, Kolongo, Mwaliza, Jangalu, na  Tamimu.

Abdallah Merey ALI MAUMBA pekee mara ya mwisho nilikutana nae Hong Kong 2009... niliongea nae na kumuuliza swali kwa nini aliacha mpira bongo na hali alikua hakuna kama yeye? alitakiwa acheze timu moja na akina Zidane... alinijibu kuwa hajuti na uamuzi aliofanya wa kuacha mpira ni sahihi kwake....

Selemani Mohamedi Mohamedi mh ALLY MAUMBA alikuwa mtu mwengine natamani anbgekuwepo sasa

Razak Careca Uwezo wa ally maumba haujawahi kutokea kwa sasa alipofika uturuki aliwai kufanya mazozi nazani ilikua fanabache na alikubalika ila alikua anapita tu anakwenda kutafuta maisha mbele hakutaka kukaa hapo maumba anayumba kulia na kushoto mbele yuko nyuma yuko mashine mtoto wa chumbangeni historya haitofutika maisha hongera coastal 1988

Ally Kiraka Ni mchezaji pekee aliyetoka daraja la 4 na kuja kupandishwa 1kwa1 daraja kwa kwanza kipindi hicho ilikua hamna premier leaque!na alitokea maumau ya chumbageni!hii ni kwa uwezo wake alojaaliwa na mungu.

Ally Kiraka Azizi peti na salim buma ndo walikua viongozi wa mau mau na walikubali kumpeleka COASTAL UNION 1kwa1 kwa kua wao walijua uwezo wa ALI MAUMBA anafaa kucheza ligi kubwa!na alikua na kipaji,hata ahmed amasha alikua ni midifield bora tanzania lakini alikua akisema m2 ninaemuogopa hata kumsogelea ni ali maumba anapokua na mpira anaweza kukufanya jambo lolote la mshangao anapokua na ball!

Razak Careca Halo kiraka wajua sikuile coastal walipoifunga simba goli 4 refa akakubali 2 mimi na maumba hatukuepo tulikua tuko shellsheli na timu ya vijana ya tanzania wenzetu tuliokua nao walikua wanatuonea wivu sisi kwasababu yakua timu nzuri timu bora hata cochi wetu mohamed msomali akawa anaipenda coastal kwahiyo sizani kama coastal ya maumba mwakuluzo mwameja mgunda kasa kolongo doglas lazaro kolongo napil jangalu mwaliza agrey abubakari
Ally Kiraka Alipoondoka tanzania aliamua kwenda ulaya!na kwa sasa anaishi ITALY!na bado anaipenda coastal union!na niwaambiavyo yupo kwenye hii group ila ana2mia jina lingine!

Ally Kiraka Mechi pekee aliyowahi kufunga goli ali maumba ilikua ni bukoba alifunga goli la kichwa!hapo ni baada ya yassin napili kuachwa tanga na sentahafu akapewa mikoba abdallah tamimu mdaula.

Ally Kiraka Razak hiyo mecho 2lowapiga simba naikumbuka kama leo nilikuwapo!na refaree hadi leo nilimuhifadhi jina alikua ni abdul kawambwa,aliwabeba sana simba ila kwa uwezo walokua nao kina mgunda na mwakuluzo walikua hawashikiki,ilibidi edward chumila alivyoona simba sasa imezidiwa na ndipo alipomfuata refa na kumwambia kwani we refa huumalizi huu mpira?cc 2mechoka bwanaa!!FAT walimfungia refa abdul kawambwa,yaani kama leo yanijia ile mechi.

Razak Careca Maumba hawezi kusahaulika yeye ndio chachu ya ushindi alikua anajua sana mpira hatasijui nisemeje mana narudisha akili nyuma naona ni kama juzi naona jinsi anavyowapiga makanzu kina gagarino na kina athuman china ilikukua burudani ya ajabu sana hata ulaya hawana uwezo ule ila nikipaji alichopewa na mungu kwasasa hakuna tena
Ally Kiraka Ni mchezaji pekee aliyefananaishwa na farasi mweupe kwa maringo yake ya uchezaji mpira!kinanda alikua akiumiza kichwa sana akiambiwa maumba ni majeruhi na ndipo alipoamua ngulungu kumchezesha no.ya maumba na alikua akifit!
Razak Careca Simba walikua wanaomba mpira umalizike nakama mimi na maumba tungekuepo sijui ingekueje mana ingekua 10 . lakini pia kukosekana kwetu pia palikua hapaja aribika kitu kulikua na agrey chamba na kasimu mwajeki kwajula ilikua si timu ya kucheza ligi ya tanzania

Ally Kiraka Razak mpaka juzi nilikwenda kwa muchachu dar ya ya kupiga mishkaki ye akiiniita we coastal union!katika maongezi ananiambia coastal union walikua waki2tesa sana!nikamkumbushia hii mechi ya refa kukataa magoli kama mvua ananiambia ile ckuile ctaisahau k...

Razak Careca Hakuna kisicho wezekana timu tunayo nzuri sana kilichobaki ni umoja na mshikamano na kuwahamasisha wachezaji wetu majungu na masufuria yasiwe na nafasi mwenye majungu aende simba au yanga hapa coastal mbele kwa mbele akiingia yanga tuna mchapa simba ndio kabisa nyingi mwaka wetu asietaka ukweli aende yanga na simba hapa ni kufa kupona piga ua mungu ajaliapo watatukoma mwaka huu


COASTAL UNION
10TH SEPT,2013

1 comment:

  1. Razak Yusuf Careca, ni katika watu nawakubali katika hii game. Uliwatesa sana mabeki wa timu pimzani na kuchangia sana ushindi na ubingwa wa Coastal union. Hongera sana kaka...

    ReplyDelete