Tuesday, March 12, 2013

Habari Picha mchezo wa jumapili simba Vs Coastal Union ambapo tulilala 2-1.

 Twaha Ibrahim 'Messi' akitafuta njia za kumtoka Nassor 'Cholo' wa Simba huku Abdi Banda akiwa tayari kumpa msaada Ibrahim.

 AAaaaaaaaaa Mohammed Miraji akikimbilia mpira huku Mohammed sudi akiwa amekata tamaa...

 Wachezaji wa Simba walikuwa wanakaba watatu watatu baada ya kipindi cha pili kuanza maana walielemewa sana na vijana wa coastal ila tatizo umaliziajiiiii.....

 Barbossa alikuwa hataki mchezo, ingawa alitoka eda ya kadi nyekundu aliyoipata Kagera lakini hakujali.

 Dhaira golikipa wa Simba akidaka mpira uliopigwa kwa kichwa dhaifu na Gabriel Barbossa.

 Hamad Juma 'Basmat' alikipiga sana katika mechi hii ingawa aliniudhi dakika za mwanzo kipindi cha kwanza alikosa goli yeye na kipa.


 Castro Mumbala alieingia kipindi cha pili alijitahidi sana kuleta mishemishe katikati ingawa mambo hayakuwa mazuri.

 Shomari kapombe alikuwa na kazi kubwa ya kuwadhibiti wachezaji wa Coastal Union wasivuke ngome yake.

Huyu ni mchezaji wa Simba Jonas Mkude, Aliumia pamoja na philip Mugenzi, alipoteza fahamu kwa dakika tano. ingawa baadae alizinduka ila hakuweza kuendelea na mchezo.

picha zinaendelea...

Sunday, March 10, 2013

Simba wameanza kufufuka baada ya kutembelewa Hospitali na Coastal Union. Matokeo Simba SC 2-1 Coastal Union SC.

Coastal Union wameendelea kujikita katika nafasi ya nne ya msimamo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya kupoteza mchezo wa leo dhidi yaa wekundu wa msimbazi Simba kwa bao 2-1 uwanja wa Taifa jijini.

Simba wamerejesha matumaini baada ya kamati ya ushindi inayoongozwa na malkia wa nyuki Rahma El Kharoos, kuzaa matunda kwa kushinda mechi ya kwanza katika nane walizopanga mkakati wa kushinda.

Wagosi wa kaya wana haki ya kujilaumu kutokana na kupoteza nafasi nyingi za wazi hasa baada ya Simba kuchezesha kikosi cha pili ikiwa ni mikakati yao ya kuepuka kuhujumiwa. Lakini mabao mawili ya harakaharaka yaliyofungwa na mshambuliaji hatari Mrisho Ngassa dakika ya 47 na Haruna Chanongo dakika moja baadae kabla ya refa kupuliza kipenga cha kukamilisha kipindi cha kwanza, yalivuruga kabisa ndoto za wagosi wa kaya kupaa nafasi moja juu..

Coastal Union walikwenda mapumziko wakiwa kichwa chini wakiwa nyuma kwa magoli mawili hali iliyomfanya kocha Hemed Morroco kuzungumza maneno makali katika vyumba vya kubadilishia hali iliyoamsha ari ya ushindi kwa vijana wa Tanga.

Razak Khalfan, alifunga bao la kwanza dakika ya nne tu baada ya kipenga cha kipindi cha pili kuanza baada ya kazi nzuri ya Ibrahim Twaha 'Messi' ambae aliingia kipindi cha pili. hivyo matokeo kubadilika na kuwa 2-1.

Wachezaji walioanza kipindi cha kwanza Coastal Union ni: Shaaban Kado, Hamad Juma, Abdi Banda, Philip Mugenzi, Mbwana Kibacha, Razakh Khalfan, Mohammed Sudi, Suleiman Kassim 'selembe', Joseph Mahundi, Danny Lyanga na Gabriel Barbosa.

kipindi cha pili alitoka Joseph Mahundi na Danny Lyanda, nafasi zao zikachukuliwa na Castro Mumbala na Ibrahim Twaha 'Messi'.

Kikosi cha Simba kilikuwa ni Abel Dhaira, Nassor Masoud 'Cholo', Miraji Adam, Hassan Khatib, Shomari Kapombe, Jonas Mkude, Amri Kiemba, Rashid Ismail, Abdalllah Seseme, Haruna Chanongo, Mrisho Ngassa.

Kwa matokeo ya leo Simba wamejiongezea point tatu na kuwa juu zaidi nafasi ya tatu kwa point 34, wakiwaacha wagosi wa kaya wakiwa na point zao 31 katika nafasi ya nne huku wakiwa na mashaka kuendelea kubaki katika nafasi hiyo kwani timu za Kagera Sugar yenye point 31, Mtibwa Sugar point 31 na Ruvu Shooting point 30 wanaimezea mate nafasi ya nne aliyokuwa nayo Coastal Union. 

COASTAL UNION
costalunion@gmail.com
10 March,2013
Dar es Salaam, Tanzania.


Saturday, March 9, 2013

Coastal Union inashuka dimbani na Simba kesho uwanja wa Taifa Dar es Salaam, ikiwa katika msimamo huu.



Pos.
Logo
Club
P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts
1
Young Africans FC
19
14
3
2
35
12
23
45
2
Azam FC
19
11
4
4
32
16
16
37
3
Simba SC
18
8
7
3
26
15
11
31
4
Kagera Sugar FC
20
8
7
5
21
17
4
31
5
Mtibwa Sugar FC
20
8
7
5
22
18
4
31
6
18
8
6
4
21
16
5
30
7
Ruvu Shooting Stars
18
8
4
6
21
18
3
28
8
20
6
7
7
20
22
-2
25
9
20
7
3
10
14
18
-4
24
10
19
4
8
7
10
14
-4
20
11
20
3
8
9
10
19
-9
17
12
Toto African
21
3
8
10
16
29
-13
17
13
JKT Ruvu Stars
18
4
4
10
14
29
-15
16
14
African Lyon FC
20
3
4
13
13
32
-19
13

Friday, March 8, 2013

Simba waunda kamati maalum ya ushindi kabla ya kukutana na Coastal Union.

 Kaimu Makamu mwenyekiti wa Simba Joseph Itangale 'Mzee Kines' akiwa na baadhi ya wajumbe mbalimbali wa Simba kwenye mkutano na wanahabari katika jengo la Simba mtaa wa msimbazi leo mchana.

 Mzee Kines akisisitiza jambo wakati akizungumza na wanahabari kuhusiana na sakata la kujiengua baadhi ya viongozi wa Simba na matokeo mabaya ya timu hiyo kwa mechi za kitaifa na kimataifa.

Kocha msaidizi wa Simba Jamhuri Kihwelu 'Julio' akizungumza na wanahabari kuhusiana na mechi ya jumapili dhidi ya Coastal Union kutoka Tanga.


Mabingwa watetezi ligi kuu ya vodacom Tanzania bara Simba SC, wameunda kamati maalum ya ushindi iliyo chini ya uenyekiti wa malkia wa nyuki El Kharus kabla ya kukutana na wagosi wa kaya siku ya jumapili hii.

Akitoa taarifa hizo ofisi za timu hiyo mtaa wa msimbazi katika mkutano na waandishi wa habari mchana huu kaimu makamu mwenyekiti Joseph Itangale ;Mzee kines’ alisema baada ya kujiengua makamu mwenyekiti Godfrey Nyange ‘Kaburu’ na mwenyekiti wa kamati ya usajili Zacharia Hans Poppe timu ya Simba bado ipo imara ya tayari imeunda kamati ya ushindi.

“Sisi hatuna matatizo, hao walioamua kujiondoka kwenye uongozi watabaki wanachama wa kawaida na kwa kudhihirisha hilo leo jioni tutakwenda kurudisha uhusiano wetu na tawi la mpira pesa.

“Timu ipo imara na tutahakikisha mechi nane zilizobaki kukamilisha msimu Simba tunashinda zote chini ya kamati ya ushindi inayoongozwa na Rahma Al Kharoos,” alisema mzee Kines.

Nae kocha msaidizi wa Simba Jamhuri Kihwelu ‘Julio’ amesema timu yake imejiandaa vizuri na anawaahidi mashabiki wa Simba wasivunjike moyo na matokeo mabaya, kwani kujiuzulu siyo dawa ya kuondoa matokeo mabaya.

“Nimesikia Coastal Union wanasema watatufunga mapema wana haki ya kusema hivyo maana nao wapo ligi kuu na sisi tutacheza mpira mzuri maana wachezaji wote 25 wapo katika hali nzuri na 11 watakaopata bahati ya kuanza kikosi cha kwanza tuna hakika watacheza vizuri.

“Sote tunamtegemea Mungu na tunamuomba, kubahatika ama kutobahatika yote ni mipango yake. Hakuna haja ya kumlaumu Mungu kwa matokeo mabaya maana kuna watu wanamuomba Mungu tangu wamezaliwa lakini hawajawahi kuokata hata laki moja lakini hawakati tamaa,” alisema Julio.

Julio aliongeza “Mimi ndie kocha bora baada ya kufariki Mzirai na kama huamini angalia timu zote nilizowahi kufundisha namna mafanikio waliyopata. Hivyo najiamini na ninaamini mechi ya Coastal Union tutashinda.”

Timu ya Simba itacheza na Coastal Union kutoka Tanga katika uwanja wa taifa siku ya jumapili tarehe 10 mwezi huu katika mechi ya ligi kuu ya voadacom Tanzania bara ambapo mshindi wa mechi hiyo ndie atakaeshika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi wenye timu 14.

Simba inacheza mchezo wake wa 19 wakiwa na historia ya matokeo mabaya hivyo mashabiki wa soka Tanzania wanaamini wekundu hao wa mtaa wa msimbazi walioanza kucheza soka mwaka 1936 wana kazi kubwa ya kurudisha heshima yao kisoka na kutetea ubingwa walioupata msimu uliopita.

COASTAL UNION
8 March, 2013
Dar es Salaam, Tanzania  

Coastal Union kukutana na Simba iliyovurugwa...


Timu ya Coastal union ya Tanga itashuka dimbani siku ya jumapili tarehe 10 mwezi huu katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kukutana na Wekundu wa Msimbazi Simba kwenye mechi yao ya 20 mzunguko wa pili ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara.

Simba inamenyana na wagosi wa kaya ikiwa imepata matokeo mabaya kwa mechi takriban tano za ligi kuu na kombe la mabingwa Afrika hivyo kufanya viongozi wake kuweweseka na baadhi wameshaanza kujiengua katika nafasi zao.

Mwenyekiti wa Coastal Union Hemed Hilal ‘Aurora’ ameieleza blog hii kuwa timu yake imejipanga vizuri kucheza kandanda la uhakika na watahakikisha wanaonyesha soka safi mbele ya mashabiki wa Kagera Sugar na Mtibwa Sugar ambao wanaiwania nafasi ya nne.

‘Najua timu ya Kagera Sugar na Mtibwa Sugar zipo Dar es Salaam kwa sasa, na watakuja uwanjani kuangalia mechi hii muhimu ambayo itaamua mtu atakaeshikilia nafasi ya tatu. Lakini watambue ingawa wao wanawania nafasi ya nne ambayo tumeishikilia kwa sasa, basi siku ya jumapili wajiandae kuitafuta nafasi ya tatu ambayo tutakuwa tumeishikilia,” alisema Aurora ambae yupo njiani na timu kuelekea mahali watakapoweka kambi mpaka siku ya jumapili.

Aurora aliongeza kuwa “Ingawa katika mechi dhidi ya Simba tutamkosa kiungo wetu mahiri na nahodha wa timu Jerry Santo kutokana na majeraha aliyoyapata katika mechi dhidi ya Ruvu Shooting lakini tunawahakikishia soka safi wapenzi wa Coastal Union.”

Alipoulizwa kuhusu kuchafuka kwa hali ya hewa Mtaa wa Msimbazi kutokana na kupoteza michezo mingi mfululuzo kutaweza kuwa ni mwanya kwa wagosi wa kaya kuwafunga Simba Aurora alisema, “Siwezi kusema ni mwanya kwetu lakini ninavyofahamu Simba ni timu nzuri lakini nasi tunajivunia uongozi safi tulionao na wachezaji wanapata kila kitu hivyo kwa upande wetu tupo vizuri ila kwa upande wa Simba siwezi kuzungumza chochote.”

Coastal Union ipo nafasi ya nne ikiwa na point 31 baada ya kucheza mechi sita katika mzunguko wa pili ambapo wameshinda mechi mbili, dhidi ya Mgambo Shooting na JKT Oljoro, wametoa suluhu tatu dhidi ya Tanzania Prison, Toto African na Ruvu Shooting, halafu wakafungwa mechi moja dhidi ya Kagera Sugar.

Baada ya kucheza na Simba siku ya jumapili Coastal Union itabakisha mechi sita ambazo ni Mtibwa Sugar, African Lyon, JKT Ruvu, Azam FC, Young Africans na Polisi Morogoro.

Timu ya Simba leo watakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia suala la kujiuzulu mjumbe wa kamati ya utendaji na mwenyekiti wa kamati ya usajili Zacharia Hans Poppe, na makamu mwenyekiti wa klabu hiyo Godfrey Nyange ‘Kaburu’.

Blog yako itafika katika mkutano huo leo kwenye jengo la klabu hiyo mtaa wa Msimbazi Kariakoo na itakuletea picha na habari kamili kuhusiana na mustakabali wa ‘Simba iliyovurugwa’.

COASTAL UNION
8 March, 2013
Dar es Salaam, Tanzania