Sunday, February 16, 2014

JKT Ruvu Vs Coastal Union, mijipicha


















COASTAL Union  imelala bao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara jana alasiri.
Bao hilo lililofungwa dakika ya 80 kwa kichwa na Said Dilunga alieunganisha mpira wa kona uliomshinda nguvu mlinda mlango wa Wagosi, Shaaban Kado.
Mchezo wa jana ulianza kwa Ruvu Shooting kuchezewa mpira wa nguvu kwa dakika 15 za awali hali iliyoamsha ari ya mashabiki wa Wagosi waliohudhuria kwa uchache lakini kelele zao zilizizima uwanja mzima na kuwafanya maafande wa Jeshi la Kujenga Taiafa kujikunyata mithili ya kuku alienyeshewa na mvua.
Hali ilibadilika ilipofika dakika ya 17 baada ya Ruvu kufanya shambulizi la kushtukiza hali iliyowashtua mashabiki wa Wagosi na kigoma kuzima hafla, lakini uimara wa Shaaban Kado uliwasaidia kuendelea kushangilia.
Dakika ya 30, Kocha Yusuf Chipo alifanya mabadiliko akamtoa Mohammed Sudi na kuingia Abdi Banda. Dakika mbili baadae Haruna Moshi Boban, almanusra awainue mashabiki wa Wagosi baada ya kubaki yeye na golikipa lakini akagongesha mwamba wa juu na mpira kudakwa kuilaini na mlinda mlango wa Ruvu.
Kabla ya mchezo kuisha mwamuzi wa jana Hashim Abdallah kutoka Dar es Salaam alimuonyesha kadi ya njano Boban bada ya akupishana nae kauli. Dakika moja kabla ya mapumziko mwamuzi alimuonyesha kadi ya njano Danny Lyanga baada ya kucheza madhambi lakini Danny alionyesha kukerwa na kadi hiyo akawa anabishana na mwamuzi, lakini hafla akatoa kadi nyingine ya njano kwa Abdi Banda kwa madai kuwa alimtolea kauli chafu.
Hivyo kipyenga cha mapumziko kilipopulizwa mashabiki wa Wagosi walimjia juu mwamuzi wa leo wakimshutumu kwa kufanya maamuzi mabaya hali iliyowavunja nguvu wachezaji wao.
Kipindi cha pili dakika ya 52 mwalimu Chipo alimtoa Yayo kato akaingia Kenneth Masumbuko, ambae kwa kiwango kikubwa aliubadilisha mchezo ukawa na kasi iliyosaidia kuingia kwenye lango la Ruvu ingawa bahati haikuwa ya Wagosi.
Dakika ya 60, Wagosi walipata kona iliyochongwa na Othman Tamim ambao uliguswa kidogo na mchezaji wa Wagosi ukagonga mwamba wa juu na kugusa mstari, kulitokea mabishano ya sekunde chache lakini mwamuzi akasema si bao.
Ilipotimu dakika ya 70, Kocha Chipo alimtoa Suleiman Kassim ‘Selembe’ akaingia Ayoub Semtawa ambae alijitahidi kumiliki mpira ili kupunguza presha ya wachezaji wa Ruvu wlaioonekana mwiba katika ngome ya Wagosi.
Aidha baada ya bao kuingia Wagosi walijitahidi kujitutumua ili kusawazisha lakini mabeki wa Ruvu walikuwa makini kuhakikisha hawapotezi nafasi ya kurudi juu kwenye ligi.
Kutokana na matokeo hayo Wagosi watashuka nafasi mbili chini kutoka ya tano mpaka ya saba, kwasababu timu nne zilizofungana point yaani Coastal Union, Ruvu Shooting, Kagera Sugar na Mtibwa Sugar jana zilishuka dimbani.
Wagosi wamepoteza mchezo wa jana hivyo wamebaki na point zao 22, Mtibwa Sugar nao wamepoteza dhidi ya Tanzania Prisons na kubakia na point 22, huku Kagera Sugar waliotoka sare na Ashanti wakiambulia point moja hivyo kupata point 23.
Ruvu Shooting wamekuwa nafasi ya tano wakijizolea point 25, ya sita inashikiliwa na Kagera Sugar wakiwa na point 23, Coastal Union nafasi ya saba point 22 na Mtibwa Sugar kutupwa nafasi ya nane point 22.
Mechi ijayo ya Coastal Union, itachezwa katika uwanja wa Mkwakwani siku ya Jumamosi Februari 22 dhidi ya Mbeya City.
Kikosi cha jana: Shaaban Kado, Mbwana Kibacha, Othman Tamim, Juma Nyoso, Yusuf Chuma, Jerry Santo, Dany Lyanga, Mohammed Sudi, Yayo Kato, Haruna Moshi ‘Boban’ na Suleiman Kassim ‘Selembe’.
Sub: Said Lubawa, Abdi Banda, Mohammed Miraji, Kenneth Masumbuko, Ayoub Semtawa na Behewa Sembwana.
COASTAL UNION
16 FEBRUARI, 2014

Sunday, February 9, 2014

Rhino Rangers Vs Coastal Union (0-1)



Baada ya ushindi wa leo katika mechi kati ya Rhino Rangers na Coastal Union kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora, ambapo Jerry Santo aliipatia Coastal Union bao la mapema dakika ya pili, sasa tumepanda mpaka nafasi ya tano.
Kwa mujibu wa msimamo wa ligi, Coastal Union kabla ya ushindi wa leo walikuwa na point 19 katika nafasi ya saba. Baada ya Mtibwa Sugar kupoteza mchezo wake dhidi ya Mbeya City, wameendelea kubaki na point 22, ambazo Coastal pia wamezifikia hivyo kuwafanya kushuka nafasi moja chini kutokana na tofauti ya mabao ya kushinda na kushindwa.
Hivyo habari njema kwa mashabiki wa Coastal Union, ni kuwa kwa sasa tunaendeleza wimbi la ushindi ili kujeweka katika nafasi nzuri hasa ikizingatiwa kocha ameamua kufanya mabadiliko ya kikosi chake ili kupata ushindi kila mechi inayokuja.
Anaeshika nafasi ya kwanza ana point 36, na sisi kutokana na mechi tisa tulizobakisha ikiwa tutashinda zote tutakuwa na jumla ya point 49. Kwa maana hiyo uwezekano wa kumaliza nafasi tatu za juu upo ikiwa tutafanya vizuri katika mechi tisa tulizobakisha ambazo ni dhidi ya:
Simba, Kagera Sugar, Azam FC, Mgambo JKT, JKT Ruvu, Ruvu Shooting, Ashanti, Mtibwa Sugar na Mbeya City.  
Ikumbukwe kuwa mechi tatu za awali kabla ya leo kukutana na Rhino Rangers tulivaana na JKT Oljoro (1-1), Yanga (0-0) na Tanzania Prisons (0-0).
Kikosi leo kilichokutana na Rhino Rangers kilikuwa hivi: Shaaban Kado, Mbwana Kibacha, Othman Tamim, Yusuf Chuma, Juma Nyoso, Jery Santo, Suleiman Selembe, Mohammed Sudi, Crispian Odula, Haruna Boban na Danny Lyanga.
Na huu ndio msimamo wa ligi Kuu Tanzania Bara baada ya mechi za leo jioni.

Top of Form
Bottom of Form
Pos.
Logo
Club
P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts
1
Azam FC
16
10
6
0
29
10
19
36
2
Young Africans FC
16
10
5
1
34
12
22
35
3
http://www.azamfc.co.tz/sites/default/files/imagecache/team_logo_tiny/mbeya%20city.jpg
17
9
7
1
23
13
10
34
4
Simba SC
17
8
7
2
32
15
17
31
5
http://www.azamfc.co.tz/sites/default/files/imagecache/team_logo_tiny/Picture%204_0.png
17
4
10
3
11
7
4
22
6
Mtibwa Sugar FC
17
5
7
5
23
21
2
22
7
Kagera Sugar FC
17
5
7
5
17
18
-1
22
8
http://www.azamfc.co.tz/sites/default/files/imagecache/team_logo_tiny/shooting_0.jpg
15
4
7
4
16
16
0
19
9
JKT Ruvu Stars
15
6
0
9
13
19
-6
18
10
http://www.azamfc.co.tz/sites/default/files/imagecache/team_logo_tiny/Logo_Ashant%2011i.jpg
16
3
4
9
15
27
-12
13
11
JKT Mgambo
17
3
4
10
8
27
-19
13
12
http://www.azamfc.co.tz/sites/default/files/imagecache/team_logo_tiny/oljoro.jpg
16
2
6
8
10
25
-15
12
13
http://www.azamfc.co.tz/sites/default/files/imagecache/team_logo_tiny/JKT_0.jpg
16
2
5
9
9
20
-11
11
14
http://www.azamfc.co.tz/sites/default/files/imagecache/team_logo_tiny/Prisons_FC.jpg
14
1
7
6
6
16
-10
10

Coastal Union
9 Februari, 2014