Sunday, November 17, 2013

Coastal Union U20 yaanza vema michuano ya Uhai.

 Yusuf Chuma (mwenye shati la mistari) akiangalia wenzake wakimenyeka leo asubuhi. Yusuf Chuma ni miongoni mwa mabeki walioingarisha Coastal Union U20 tangu mwaka juzi akishirikiana na Nzara Ndaro, Abdi Banda na Hamad Juma. kwa sasa Chuma, Banda na hamad wamepandishwa timu ya wakubwa. Alikuja kuwaangalia wenzake baada ya Ligi Kuu kusimama.

 Nzara Ndaro akiangalia wa kumpa mpira katika kipindi cha kwanza wakati huo timu imelala 1-0.

 Ayoub, beki mbili wa Coastal Unio  akitoa pasi kwa Raizin Hafidh (namba nne) huku Nzara Ndaro (nahodha wa Coastal) akiangalia kwa makini.

 Kiungo mshambuliaji wa Coastal Union Ally Ufudu akikokota mpira kuelekea lango la Azam.

 Yusuf Chippo akiwajibika uwanjani, hapa anawakemea vijana wake wasicheze mipira ya juu.

 Tunakwenda moja moja, ndiyo staili ya kocha Yusuf Chippo.

 Balaaaa... mchezaji mmoja anakabwa na kijiji.

 Penalt hii iliyoingizwa kimiani na Raizin Hafidh 'Boban' dakika ya 50 baada ya mchezaji wa Azam kuunawa mpira katika eneo la hatari.

 Wachezaji wa Coastal Union wakishangilia bao la kwanza lililofungwa kwa mkwaju wa penalt dakika ya 50.

 Nao ni na...

 Raizin Hafidh 'Boban' akiwa ameshampiga chenga golikipa wa Azam, anaelekea kupiga shuti kwa guu lake la kushoto kuhitimisha kilio kwa Azam dakika ya 55.

 Wachezaji wa Coastal Union wakishangilia bao la pili lililofungwa na Raizin Hafidh 'Boban'.

 Raizin Hafidh 'Boban' akitafuta mbinu za kumtoka mchezaji wa Azam huku mchezaji wa Coastal akiwa tayari kutoa msaada.



Kocha wa Coastal Union, Yusuf Chippo akizungumza na kiungo wa timu hiyo Ally Ufudu wakati mechi ikiendelea, leo asubuhi uwanja wa Karume Ilala jijini.
 

TIMU ya Coastal Union chini ya miaka 20 imeanza vema michuano ya UHAI U20 baada ya kuwachapa mahasimu wao wa muda mrefu Azam FC kwa mabao 2-1 yaliyoingizwa kimiani na kijana
Ilikuwa ni dakika ya 50 kipindi cha pili baada ya mchezaji wa Azam kuunawa mpira katika eneo la hatari Raizin Hafidh ‘Boban’ akakabidhiwa mikoba ya kupiga mkwaju wa penalt ambao ulitikisa nyavu za Azam huku golkikipa wa timu hiyo akibaki chini ameshangaa.
Bao hilo liliamsha shangwe katika uwanja wa Karume uliopo Ilala jijini Dar es Salaam, hali iliyoonyesha watazamaji wengi walikuwa upande wa Coastal Union.
Baada ya bao hilo kuingia wachezaji wa Azam walipoteza mwelekeo na kuruhusu mashambulizi ya mara kwa mara langoni mwao hali iliyompa mwanya ‘Boban’ ambaye alitokea upande wa kulia akamramba chenga beki wa Azam akaingia kwenye box dogo akakutana na golikipa wa Azam amezubaa, naye akamramba chenga na kumalizia kazi nzuri iliyotokana na juhudi zake binafsi kwa mguu wa kushoto.
Kuingia kwa bao la pili kulimaanisha kitu kimoja tu kwa Azam, kuhakikisha mvua hiyo ya mabao haiendelei. Hivyo wakaanza kucheza mchezo wa kujihami hali iliyowafanya kuendelea kushambuliwa mara kwa mara.
Hata hivyo wachezaji wa Coastal Union nao wakaanza kujisahau na kucheza kwa kujiamini huku wakionekana kuridhika na mabao hayo. Kutokana na mchezo huo ulioonyesha dharau na kujiamini vijana hao ambao mwaka jana walitawazwa kuwa kikosi bora cha michuano hiyo, walikosa mabao mengi ya wazi yaliyosababishwa na uzembe wa mabeki wao.
Katika kipindi cha kwanza Azam ambao ni mabingwa watetezi wa michuano hiyo baada ya kuwatoa Coastal Union mwaka jana walipata bao la mapema katika dakika ya 3 mfungaji akiwa Erick Haule, aliyetumia vema makosa ya mabeki wa Coastal Union na kumalizia krosi iliyopigwa kutoka upande wa kulia ikamkuta miguuni na kumbabatiza golikipa wa Coastal Union kasha ukaingia wavuni.
Bao hilo lilidumu mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza huku vijana wa Coastal Union wakiomba kipindi hicho kiishe mapema kutokana na mashambulizi waliyokuwa wakiyapata kutoka kwa wapinzani wao.
Katika hatua nyingine, ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Azam FC ndiwo ushindi wa kwanza kwa Coastal Union chini ya miaka 20 kwa vijana wenzao hao tangu walipoanza kukutana miaka minne iliyopita.
Aidha kwa mara tatu mfululizo Azam wamekuwa wakiwashinda Coastal Union kwa mikwaju ya penalt kwenye hatua ya mtoano, baada ya kutoka suluhu kwenye dakika za kawaida.
Kundi A lina timu nne za Coastal Union, Azam FC, Yanga na Mbeya City. Matokeo ya mechi inayochezwa sasa kati ya Yanga na Mbeya City ndiyo yataihakikishia Coastal Union kuongoza kundi kabla ya kutupa karata yake ya pili siku ya Jumanne dhidi ya Yanga katika uwanja wa Karume Ilala saa mbili asubuhi.
COASTAL UNION
NOV 17, 2013
DAR ES SALAAM, TANZANIA

No comments:

Post a Comment