Tuesday, November 26, 2013

Coastal Union yafanya kama ilivyofanya Arusha...


 Hawa jamaa wa Azam TV wametuchelewesha sana kuanza mechi.....

 Alitupiwa, akaipokea vizuri Mohammed Rajabu......

 Alipokunjuka akakutana na kigingi....

Ufuuuduuu vipi?

                                                       Furaha ya ushindi lazima ucheze ndombolo.

 Kipanga kila alipopokea mpira, pembeni yake alikuwa na wachezaji watatu wa JKT Oljoro. Huyu kijana yupo vizuri sana, aangaliwe kwa jicho la kulelewa kisoka.

Hapa Kocha Mkuu wa timu ya Viajana, Joseph Lazaro akizungumza na vijana wake, vipi jamaaani?
                                    Kosakosa langoni mwa Coastal Union hazikukosekana.

                                Leo Kipanga alikabwa na wachezaji watatu dakika zote.

 Nahodha wa Coastal Union, Nzara Ndaro akizungumza na vyombo vya habari kuhusu mechi ya leo.

                   Nahodha Nzara Ndaro akiwasalimia mashabaki kuwashukuru baada ya mechi.

                               Safari ya kuelekea Arusha ilianzia Chamazi baada ya mechi.

MNAMO dakika ya 6 ya kipindi cha kwanza baada ya kulisakama lango la JKT Oljoro kwa takriban dakika tatu mfululizo, wachezaji Ayoub Semtawa na Mtenje Albano walipigiana pasi nje kidogo ya eneo la kujidai golikipa wa Oljoro.

Baadaye Juma Mahadhi akawazidi ujanja mabeki wa Oljoro akapokea pasi murua kutoka kwa Mtenje ambaye alijifanya kama anapiga mabeki walipogeuka akampa Mahadhi ambaye aliukokota mara mbili akainua uso kumuangalia golikipa amekaa upende gani, akakunjuka shuti kimo cha paka upande wa kushoto ukapuchua mwamba na kuzama ndani.

Baada ya bao hilo Oljoro walijitahidi kujibu mashambulizi lakini mabeki wa Coastal Union, walikuwa imara kumlinda golikipa wao.

Hata hivyo vijana wa Wagosi wa Kaya walikosa nafasi nyingi katika kipindi cha kwanza kutokana na kukosa mawasiliano baina yao na uvivu wa kuvika langoni mwa Oljoro kila zilipomiminwa krosi..

Kabla ya kipindi cha kwanza kuisha Kocha Joseph Lazaro alimtoa Abdallah Waziri akamuingiza Zungu, ambapo mpaka timu zinakeenda mapumziko bado bao lilibaki 1-0.

Kipindi cha pili kilianza kwa Oljoro kuja juu na kucheza mpira wa kasi kitu kilichoisumbua ngome ya Wagosi wakapoeza mwelekeo.

Baada ya Lazaro kuona hali mbaya akafanya mabadiliko akamtoa Ayoub Semtawa na kumuingiza Mwaita, baadaye akamtoa Ally Ufudu na kumuingiza Raizini Haji, halafu ilipofika dakika ya 31 kipindi cha pili alimtoa Juma Mahadhi na kumuingiza Batista.

mabadiliko hayo yalirudisha uhai kidogo katika kikosi cha Wagosi ambao kama si golikipa wao kuwa imara bao hilo lingerudishwa katika dakika za awali za kipindi cha pili.

Hata hivyo mpaka kipyenga cha mwisho kinapulizwa, matokeo bado yalisomeka 1-0, ambapo hali hiyo iliashiria kitu kimoja tu. JKT Oljoro wana safari ya kurudi Arusha kama si leo usiku basi kesho alfajiri baada ya kuaga michuano ya Uhai.

Itakumbukwa katikati ya mwezi huu mjini Arusha JKT Oljoro na Coastal Union walikutana katika hatua hihii ya robo fainali ya michuano ya Rollingstone Oljoro wakatolewa kwa bao 1-0. Hivyo imedhihirisha hawa ni wateja wetu.

Mechi ijayo itachezwa katika uwanja wa Azam Complex Chamazi siku ya AlhamisiNovemba 28, katika hatua ya nusu fainali dhidi ya Azam FC saa tisa alasiri.
COASTAL UNION
NOVEMBA 26, 2013
DAR ES SALAAM TANZANIA

No comments:

Post a Comment