Friday, November 22, 2013

Coastal Union yazidi kufanya vizuri kombe la Uhai

 Kikosi cha leo kilichomenyana na maafande wa JKT Ruvu katika uwanja wa Karume jioni hii na kutka na ushindi wa mabao 2-1.

 Mohammed Rajabu wa Coastal Union, huyu ndiye aliyetumbukiza mabao yote mawili na kurudisha matumaini kwa Wagosi baada ya kuchapwa na Yanga katika mechi iliyipota.

 Ramadhan Shamte wa Coastal Union akitafuta mbinu za kuunyakua mpira kutoka kwa mchezaji wa JKT Ruvu.

 Kocha Yusuf Chippo akiwaambia cha kufanya pindi waingiapo dimbani, Ally Kipanga jezi namba saba na Ayoub Semtawa jezi namba 10. Baada ya kuingia wao ndipo mpira ukabadilika na mabao yote mawili kuingia.

Mbona hamuingii/ Nimesema nyote mjae kati maana pale mipira ikiingizwa inakosa watu.....

Bao la dakika ya 69 lililotiwa kimiani na mshambuliaji wa timu B, Mohammed Rajabu ndilo lililoibua matumaini ya kuendelea na michuano hiyo baada ya kuamini mechi ya leo itaisha kwa kufungwa ama kutosa suluhu kitu ambacho kingewafungisha virago wagosi.
Ilikuwa ni piga nikupige katika lango la JKT Ruvu, ndipo Juma Mahadhi alipoudaka mpira nje ya 18 na kumpenyezea Mohammed Rajabu ambae aliwakuta mabeki wa Ruvu wamejisahau akapenya na mpira mpaka akakutana na golikipa wa Ruvu, Patrick Matui akamlamba chenga na kupiga shhuti hafifu lililotinga wavuni.
Awali katika dakika ya 49, dakika tatu tu baada ya kipindi cha pili kuanza, Thomas Ndimbo alitumia vema makosa ya mabeki wa Wagosi akaifungia bao la kuongoza timu yake hali iliyowavunja nguvu Wagosi ambao walianza vibaya kipindi cha kwanza.
baada ya bao hilo kuingia wavuni kocha wa Wagosi alikaa kama kamati na benchi lake la ufundi akawainua wachezaji wote wa akiba akiwaambia wapashe lengo likiwa ni kupiga ramli nani aingie akaokoe jahazi.
ndipo akafanya maamuzi ya kumuingiza Ally Kipanga na Ramadhan Shame. akawatoa Mohammed Issa na Hassan Amir. Baadaye akamtoa Raizn Hajji akamuingiza Mtenje Albano.
ndipo ilipofika dakika ya 88 ya mchezo Ramadhan Shame alimpenyezea mpira Mohammed Rajabu ambaye alikuwa katikati ya uwanja na kuanza kukimbizana na mabeki wa Ruvu huku golikipa akiwa langoni hajui la kufanya, alipoingia ndani ya box, Mohammed aliachia shuti kali kimo cha paka na kumpita golikipa wa Ruvu katika kwapa huku ukitinga wavuni na kuibua shangwe kwa mashabiki wa Wagosi waliojaa uwanja mzima.
baadaye mpira ulikuwa upande wa Ruvu huku kosakosa zikiwa nyingi kabla mwamuzi kupuliza kipyenga cha mwisho kuashiria mchezo huo umesiha kwa Wagosi kuibuka na mabao mawili kwa moja huku wakizoa point tatu na kufanya kuwa na jumla ya point 6.
Itakumbukwa mevhoi ya awali Coastal Union walishinda dhidi ya Azam FC 2-1, wakafungwa na Yanga bao 1-0 na leo wameshinda mabao 2-1 dhidi ya Ruvu JKT. Mechi ya mwishi itachezwa katika uwanja wa Chamazi Jumapili Novemba 24 saa mbili asubuhi dhidi ya Mbeya City.
hata hivyo mwalimu wa Coastal Union amelalamikia ratiba mbovu ya michuano hiyo kwani awali ratiba ilikuwa ikionyesha mechi ya JKT Ruvu na Coastal Union itachezwa Jumamosi Novemba 23, lakini asubihi ya leo walipokuwa wakijiandaa kuelekea mazoezini ndipo walipopata taarifa ya mabadiliko hayo.
COASTAL UNION
DAR ES SALAAM, TANZANIA
NOVEMBA 22, 2013

No comments:

Post a Comment