Tuesday, November 12, 2013

Yusuf Chippo ndiye Kocha mpya Coastal Union.

 Yusuf Chippo aliyekaa akibadilishana mawazo na kocha Joseph Lazaro, ambaye ndiye aliyekabidhiwa mikoba ya kocha aliyemaliza mkataba wake wa Wagosi, Hemed Morocco.

 Yusuf Chippo alipokuwa akisaidiana na Adel Amrouche kuifundisha Harambee Stars, timu ya soka ya Kenya.

                                                                    Yusuf Chippo.

BAADA ya aliyekuwa kocha mkuu wa Coastal Union, Hemed Morocco kumaliza muda wake na timu kuwa mikononi mwa wakongwe wa timu hiyo Joseph Lazaro na Razakh Yusuf 'Careca' sasa timu imepata mrithi atakayeinoa kuanzia Januari.

Yusuf Chippo, kutoka Kenya amesaini mkataba wa mwaka mmoja na Wagosi kukinoa kikosi hicho kilichosheheni wachezaji wenye uwezo wa hali ya juu.

Akizunumza na mwandishi wa blogu hii mara baada ya kukiona kikosi cha Wagosi kwenye mechi ya mwisho ya mzunguko wa kwanza Ligi Kuu bara, Chippo alisema "Nimeiona timu, si mbaya na ina wachezaji waliopevuka. Kuna mambo madogo sana ya kuwabadilisha na nina haakika watacheza soka nanyi mtaapara raha kama ulivyosema mnataka raha (kicheko....)."

Aidha kocha huyo ambaye aliwahi kufundisha timu kadhaa za Kenya ikiwemo Bandari ya Mombasa, Nzoia ya Bungoma, vilevie aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Ufundi (TD) wa Ulinzi pamoja na kuwa kocha msaidizi wa timu ya taifa la Kenya, Harambee Stars aliweka wazi kuwa hahitaji kuongezaa mchezaji bali haohao waliokuwepo wanaatosha kuifikisha mbali timu.

"Nilikaa kwenye jukwaa kuaangalia 'game' (Ilikuwa kati ya JKT Ruvu na Coastal Union), nimeona timu inazuia zaidi kuliko kushambulia, hiyo ni ugonjwa ya timu nyingi za TZ (Tanzania), na nitaondoa tatizo hilo wacha tuone," aliongeza Chippo.

COASTAL UNION
DAR ES SAALAAM, TANZANIA
12 NOV, 2013

No comments:

Post a Comment