Thursday, January 23, 2014

A to Z picha za safari ya leo kutoka Oman.

 Jana kulikuwa na kikao cha kujadiloi mustakabali wa timu, baada ya kambi hapa tulikuwa tunafanya majumuisho. Ofisa wa Ubalozi Mussa Abdallah aliwauliza wachezaji waseme kinachowasibu ili wakishindwa wasiwe na sababu.

 Ofisa Ubalozi wa Tanzania nchini Oman, Mussa Abdallah (kushoto), akiwa na Mwenyekiti wa Coastal Union Hemed Hilal 'Aurora' katika kikao hicho cha majumuisho ya kambi ya wiki mbili nchini Oman.

 Mussa Abdallah, Hemedd Hilal wakiwa na Meneja wa Coastal Union, Akida Machai (wa tatu kutoka kushoto) katika kikao hicho jana adhuhuri katika hoteli ya Taj Mahal jijini muscat.

 Haruna Moshi 'Boban' akichangia mada katika kikao cha majumuisho ya kambi ya wiki mbili nchini Oman.

 Nahodha wa Coastal Union, Juma Said 'Nyoso' akichangia mada katika mkutano huo uliofanyika jana.

 Meneja Akida Machai, nae alitoa lake la moyoni.

 Mwenyeji wetu ambae alikuwa daktari wa timu ya Fanja SC na timu ya taifa ya Oman, Dk. Majid akichangia mada katika mkutano huo jana.

Suleiman Kassim 'Selembe' na Yayo Kato wakiwa uwanja wa ndege wa Sultan Qaboos jijini Muscat Oman, leo asubuhi kabla ya kupaa kurejea nyumbani tayari kwa mechi dhdi ya JKT Oljoro jijini Tanga siku ya Jumamosi Januari 25.
 Viongozi wa Ubalozi, na viongozi wa Fanja SC wakipata picha ya kumbukumbu na viongozi wa Coastal Union na wachezaji katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Sultan Qaboos Jijini Muscat Oman leo asubuhi.

 Msemaji wa Coastal Union Hafidh Kido (wa kwanza kulia) akiwa na golikipa wa Coastal Union Said Lubawa (katikati) na kocha msaidizi Ally Jangalu kabla ya kuruka na ndege ya shirika la Oman Air kurudi Tanzania leo asubuhi.

 Baada ya kutua Makamu Mwenyekiti Steven Mnguto (wa kwanza kulia), Meneja wa timu ndogo Abdulrahman Ubinde, Meneja msaidizi timu kubwa Abdi Masamaki na daktari wa timu Mzee Mganga katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa JK.

 Shabiki wa Coatal Union, Omar (kushoto) akiwa na Allya Nassor 'Ufudu', Yusuf Chuma na Mbwana Hamis 'Kibacha' katika uwanja wa ndege wa JK Nyerere.

 MzeeMnguto na Masamaki wakihakikisha mizigo yote inapatikana...

 Baada ya kutua vijana waligonga chakula halafu wakaanza safari kuelekea kambini jijini Tanga.

Hii ndiyo mitaa ya Mawaleh, mitaa ambayo vijana wa Coastal Union walijidai kwa wiki mbili jijini Muscat.

COASTAL UNION
23 JANUARI, 2014
DAR ES SALAAM, TANZANIA

No comments:

Post a Comment