Wednesday, January 29, 2014

Coastal Union 0-0 Yanga



 Kocha wa Yanga (kulia) Van De Plunm akiwa na Meneja wa Yanga Hafidh Saleh kabla ya mchezo leo.


 Kocha wa Coasal Union Yusuf Chipo akihojiwa na wanahabari kabla ya mchezo.


 Abdi Banda akitafuta mbinu za kumtoka mchezaji wa Yanga, Oscar Joshua katika mchezo wa leo uwanja wa Mkwakwani.


Haruna Moshi 'Boban' akimuonyesha kocha Chipo kuwa mambo anayaweza.



                               Kenneth Masumbuko akitolewa uwanjani baada ya kuumia kipindi cha pili.

KOCHA Mkuu wa Coastal Union, Yusuf Chipo ameanza kuridhishwa na kiwango cha wachezaji wake mbali ya kutoa suluhu ya pili katika mechi za ligi kuu Tanzania Bara.
Mechi ya leo kati ya Coastal Union na mabingwa watetezi wa ligi hiyo Yanga, iliyopigwa kwenye uwanja wa Mkwakwani imeisha kwa sukuhu tasa ya bila kufungana lakini walimu wote wawili wameonyesha kuvutiwa na soka lililochezwa leo.
Yanga walianza kwa kasi huku wakilisakama lango la Wagosi wa Kaya mfululizo na kupata kona Zaidi ya nne ndani ya dakika tano za awali kipindi cha kwanza. Hali ilizidi kuwa mbaya kwa upande wa Coastal Union ambapo Yanga walionekana kuwa makini na kushambulia kwa kasi.
Dakika ya 36, Crispian Odula wa Coastal Union alikosa bao la wazi akiwa yeye na golika wa Yanga Deogratius Munishi (Dida).
Mpaka kipindi cha kwanza kinaisha hakuna mtu alieona lango la mwenzake hali iliyowapa mwanya makocha kuwapa nasaha ili wasirudie makosa waliyofanya awali.
Hata hivyo maamuzi ya leo kwa refa wa kati yalionyesha kuwakera mashabiki wa pande zote mbili halo iliyoleta taharuki na mchezo kusimamishwa Zaidi ya mara mbili ili kuweka mambo sawa.
Kipindi cha pili kilianza kwa Yanga kushambulia kwa kasi ili kupata bao moja ili kuwaharibu kisaikolojia wachezaji wa Coastal Union, hata hivyo mlinda mlango wa Wagosi, Shaaban Kado alikuwa makini langoni kuhakikisha hatari zote zinaishia nje ya eneo lake la kujidai.
Dakika tisa za awali katika kipindi cha pili Nadir Haroub ‘Canavaro’ alitaka kujifunga katika harakati kuokoa shuti la Abdi Banda. Baada ya hapo mashabiki wa Yanga wakaanza kumrushia chupa Canavaro.
Katika kipindi cha pili Yanga walianza kupoteza pumzi na kuchezewa mpira mwingi na Coastal Union, walioamka kutoka usingizini.
Hata hivyo ilipofika dakika ya 68 mwamuzi alitoa nafasi kwa Yanga kupiga mpira wa adhabu ndogo baada ya mchezaji wao kuchezewa vibaya nje kidogo ya 18. Lakini faulo ile ilionekana kuwakera wachezaji wa Coastal Union, ndipo mwamuzi akampa kadi ya njano Haruna Moshi ‘Boban’.
Baadae dakika ya 77 winga wa Coastal Union, Kenneth Masumbuko aliumia misuli ya mguu akaingia Mohammed Sudi, ilipofika dakika ya 86 alitoka Yayo Kato akaingia Mohammed Miraji (86).
Mpaka dakika 90 zinakamilika matokeo yaliendelea kusomeka hivyo hivyo 0-0. Hali hiyo ilionekana kuwakera mashabiki wa timu zote kwani Yanga bado wana kampeni ya kushikilia kileleni, huku Coastal Union wakitaka kujisafisha baada ya kutoa suluhu ya 1-1 na JKT Oljoro katika uwanja huu huu wa Mkwakwani Jumamosi iliyopita.
COASTAL UNION
29 JANUARI, 2013
TANGA, TANZANIA

No comments:

Post a Comment