Friday, January 17, 2014

Dhifa ya chakula cha usiku kasri la Masoud Esry leo usiku

Dk. Francis Mganga akicheza na farasi
 Msemaji wa Coastal Union, Hafidh Kido akipozi kwa picha kwenye banda la farasi, usiku wa leo.

Golikipa Shaaban Kado, Said Lubawa na Abdullah Othman 'Ustaadh' wakipozi na farasi.
 Wachezaji, kocha na wenyeji wetu katika jumba la Masoud Esry, mjomba wa Salim Esry mwanachama wa Coastal Union nchini Oman, wakiangalia mandhari ya kasri hiyo usiku huu.


Masoud Esry, wa kwanza kushoti akiwa na mmoja wa wanafamilia ya Esry katika chakula cha usiku alichowaandalia wachezaji wa Coastal Union, usiku wa leo.


Wachezaji pia walipata muda wa kuangalia soka, ambapo wanafamilia ya Esry wametengeneza uwanja wa soka ndani ya kasri hilo hucheza soka kila wamalizapo shughuli za kutwa nzima.
 Haruna Moshi 'Boban', akiwa na Othman Abdullah 'Ustaadh'.

 Kaka yake Salim Esry, Khalid Esry wa kwanza kulia akishughulika kuandaa chakula pamoja na wanafamilia ya Esry usiku huu.

 Kutoka kushoto, Dk. Francis Mganga na Kit Manager Mohammed wakipakua chakula katika dhifa hiyo.

Shaaban Kado kushoto akiwa na mwenyeji wetu mjomba wa Salim Esry, Mzee Masoud Esry wakipakua maakuli.
                                 Nahodha wa Coastal Union, Juma Nyoso akipiga vitu vyake.

                                           Aaaaahhhh hamadi Juma 'Basmat' akishughulika...


 Kutoka kulia Salim Esry, Boban na Ustadh wakiwa katika harakati za kupakua maakuli usiku huu.

                                  Suleiman Kassim 'Selembe' akifanya mambo ndani ya 18.

 Mahmoud Zubery 'BinZubery' (mwenye jacket jeusi, aliekaa) mmiliki wa blog ya Bongostaz, akifanya mambo katika blog yake baada ya dhifa.

 Kibacha na Nahodha wake Nyoso wakitendea haki dhifa ya leo.

Suala zima la 'self service' lilihusika sana. (kurudia imo).
Baada ya chakula mchezaji wa Coastal Union, Othman Abdullah 'Ustaadh' alipiga dua ya shukurani.

COASTAL UNION
17 JANUARI, 2014
MUSCAT, OMAN

No comments:

Post a Comment