Saturday, January 25, 2014

Coastal Union 1-1 JKT Oljoro

                      Kikosi cha leo kilichomenyana na JKT Oljoro uwanja wa Mkwakwani leo.

                   Viongozi wa Coastal Union wakifuatilia mechi ya leo uwanja wa Mkwakwani.

 Meneja wa Coastal Union akitaniana na Kocha wa JKT Oljoro Hemed Morocco kabla ya mchezo leo.

                     Atupele Green akimtoka mchezaji wa JKT Oljoro uwanja wa Mkwakwani leo.

 Kenneth Masumbuko, akitafuta mbinu za kumtoka Nurdin Mohammed wa JKT Oljoro katika uwanja wa Mkwakwani leo.

                                                             Yayo Kato Lutimba

 Yusuf Chipo, Kocha wa Coastal Union akiangalia mchezaji wake Danny Lyanga akifanya vitu vyake katika mechi ya leo uwanja wa Mkwakwani.

 Yayo Kato akijishauri cha kufanya kabla ya kuanza kukimbizana na Ally Hamza wa JKT Oljoro.

 Mfungaji wa bao la Coastal Union Yayo Kato, akigombania mpira na mchezaji wa JKT Oljoro Ally Hamza.

 Kocha Mkuu wa Coastal union, Yusuf Chipo akiwatuliza wachezaji wake baada ya kufungwa bao la kusawazisha leo.

                                             Coastal Union ina mashabiki wa mataifa mengi.

 Danny Lyanga akituliza mpira kwenye gamba katika mechi ya leo alicheza vizuri ingawa kuanguka anguka kulikuwa kwingi.

                                                                Danny Lyanga.



Wachezaji wa JKT Oljoro wakishangilia baada ya kusawazisha na kulazimisha matokeo kusomeka 1-1 leo.
 

MBALI ya kukaa Oman kwa wiki mbili lakini kikosi cha Coastal Union kimeshindwa kuwapa raha wapenzi wake katika uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga baada ya kulazimishwa suluhu na wanajeshi wa JKT Oljoro kutoka Arusha.
Suluhu ya 1-1 imeonekana kuwavunja nguvu viongozi na mashabiki wa Coastal Union, ambao waliingia uwanjani kwa idadi ndogo kutokana na tatizo la ukataji tiketi kuwakwaza baadhi ya mashabiki waliotaka kuiangalia timu yao iliyotoka Oman wiki hii.
Coastal Union walianza mchezo wa leo kwa kujiamini wakitoa pasi za uhakika huku wakifika katika lango la wapinzani wao mara kwa mara.
Ilipotimu dajkika ya 7, Yayo Kato aliandika bao la kwanza baada ya kupokea pasi murua kutoka kwa Kenneth Masumbuko baada ya Hamad Juma kufanya kazi nzuri ya kumdhibiti beki wa Oljoro na kupiga krosi.
Bao hilo lilidumu kwa dakika 45 za awali ambapo mpaka timu zinakwenda mapumziko ubao uliendelea kusomeka 1-0. Hali iliyoongeza furaha katika uwanja wa Mkwakwani huku kila mmoja akiamini kuna mabao mengi mengine yanakuja.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku wachezaji wa Oljoro wakicheza kw akujihami na kupiga pasi fupi zilizoonyesha kuwachanganya wachezaji wa Coastal Union. Hali hiyo vilevile ilimnyima raha kocha wa Coastal Union, Yusuf Chipo ambae alionekana kusimama wakati wote.
Kufikia dakika ya 75 Coastal Union, tayari walishafanya mabadiliko ya wachezaji watatu ambapo alitoka Kenneth Masumuko na kuingia Abdi Banda, baadae alitoka Othamn Tamim akaingia Crispian Odula mwisho alitoka Yayo Kato na kuingia Mohammed Miraji.
Wagosi wa Kaya waliendelea kumiliki mpira, walifanya juhudi kubwa ambapo muda mwingi Danny Lyanga alikuwa msumbufu katika winga ya kushoto hali iliyomnyima raha golikipa wa Oljoro, Mohammed Yusuf.
Ilipotimu dakika ya 87 dakika chache kabla ya mwamuzi wa leo Israel Nkongo kumaliza kipute, Hamis Saleh wa JKT Oljoro alitumia vema makosa ya mabeki wa Coastal Union na kupachika bao lililoamcha benchi la timu yake kwa furaha.
Baada ya hapo Coastal Union hawakuonekana kukata tamaa waliendelea kuzitendea haki nyasi za uwanja wa Mkwakwani kwa kusakata kabumbu la hali ya juu. Dakika ya 89 Crispian Odula alipata pasi akiwa ndani ya 18 lakini akapiga shuti hafifu lililotua ndani ya mikono ya golikipa wa Oljoro.
Mpaka mchezo unakamilika, ubao ulisomeka 1-1 hali iliyowatoa kichwa chini wachezaji na mashabiki wa Wagosi wa Kaya waliokuwa na matumaini makubwa ya kushinda.
Kikosi cha leo Coastal Union kilikuwa hivi: Said Lubawa, Hamad Juma, Othman Tamim, Juma Nyoso, Mbwana Kibacha, Jerry Santo, Atupele Green, Razakh Khalfan, Yayo Kato, Danny Lyanga na Kenneth Masumbuko.
Wachezaji wa hakiba walikuwa ni: Mansoor Alawi, Abdi Banda, Yusuf Chuma, Mohammed Miraji, Suleiman Kassim, Crispian Odula na Ayoub Semtawa.
COASTAL UNION
25 JANUARI, 2014
TANGA, TANZANIA

No comments:

Post a Comment