Sunday, July 14, 2013

Habari picha mechi ya leo nusu fainali Coastal Union Vs Azam FC.Mchezaji w



Ukisikia kivumbi na mwenzake jasho ndo hiki. Taraa.
 Ally Kipanga wa coastal Union akijitahidi kuukimbilia mpira aliotanguliziwa na Ayoub Semtawa aliye nyuma yake.

 Yooote tisa kumi mabeki wa caostal Union leo walikuwa imara sana, hapa Hamad Juma 'Basmat' akitafuta mbinu za kumtoka mchezaji wa Azam.

 Leo Ally Ufudu alifunikwa kabisa, Azam waliambiwa wamkabe sana kijana huyu. Hapa akituliza mpira huku mchezaji wa Azam akijiandaa kuenda kuuharibu.

 Baada ya dakika 90 kuisha kocha Bakari Shime akipanga mashambulizi upya kujiandaa na dakika 30 za nyongeza.

 Benchi la Coastal Union hili baada ya abdul Ubinde kupewa kadi nyekundu.

Bakari Mwaita akikimbia na mpira huku mchezaji wa Azam akiumezea mate.

                                  Ayoub Semtawa akipewa kadi nyekundu na mwamuzi wa leo.
Mchezaji wa Azam FC akipewa kadi nyekundu baada ya kumchezea madhambi Ally Ufudu.
                                           Goli alilofunga Hamad Juma ni hili katika penati ya pili.

        Mansour Alawi akishangaa mpira unaingia wavuni hii ni penati ya tano na ya mwisho tumelala kwa penati 4-5.



Coastal Union chini ya miaka 20 wameaga michuano ya Rollingstone katika hatua ya nusu fainali baada ya kutolewa na Azam FC kwa mikwaju ya penati 4-5 kwenye uwanja wa General Tyre asubuhi hii.
Mechi ya leo iliyokwenda mpaka dakika 120 baada ya dakika 90 za kaiwaida kuisha kwa suluhu ya bila kufungana, zikaongezwa dakika 30 lakini hazikusaidia kubadili matokeo kila timu ilishindwa kuchungulia nyavu za mwenzake.
Aliyeharibu furaha za wagosi wa kaya ni Mohammed Hassan aliyeingia kipindi cha pili kukosa penati ya kwanza kwa kupaisha mwamba wa juu ndipo Azam wakapata nguvu na kutumbukiza wavuni penati zote tano ingawa Coastal Union walifanikiwa kutumbukiza penati nne zilizobaki lakini hazikufua dafu.
Mchezo ulikuwa wa kukamiana lakini mashabiki wa Coastal Union wakati wote walikuwa wakitupa lawama kwa mwamuzi wa kati na wanyoosha vibendera kwa dhana kuwa wamenunuliwa na Azam FC baada ya kitendo cha kustaajabisha kabla ya mchezo kuanza Bus la Azam lilipokuwa likiingia uwanja wa General Tyre waamuzi nao walionekana wakishuka pamoja na wachezaji wa Azam.
Katika dakika 45 za mwanzo Coastal Union walikosa mabao takriban matatu baada ya mchungulia nyavu maarufu Ally Nassor Ufudi kupata nafasi tatu akiwa yeye na golikipa lakini alipaisha juu. Azam nao walikuwa wakiliandama lango la Coastal Union lakini mabeki imara wa wagosi walimhami Mansor Alawi aliyekuwa langoni mwa Wagosi.
Baada ya maamuzi ya mwamuzi wa kati Emmanuel Mwandembwa, kuwa mabaya kupita kiasi meneja wa Coastal Union, Abdulrahman Ubinde aliingilia kati na kuzungumza na mkutugenzi wa michuano aliyetambulika kwa jina moja la Wilbroad lakini Wilbroad alimweleza mwamuzi amuondoe jukwaani Ubinde kwa maelezo kuwa anafanya vurugu.
Kipindi cha pili mpira ulibadilika ambapo Azam walianza kwa kasi na kucheza madhambi ya kusudi, katika dakika ya 70 nahodha wa Coastal Union Nzara Ndaro almanusra apewe kadi nyekundu kwa kutaka kupigana na mchezaji wa Azam kutokana na madhambi ya maudhi.
Dakika kumi kabla ya mchezo kuisha  Ayoub Semtawa alionyeshwa kadi ya njano, kwakuwa alikuwa na kadi nyingine hivyo ikawa ni nyekundu.
Katika dakika 30 za nyingeza mpira ulikuwa wa kukamiana na umakini wa hali ya juu, lakini mpaka nusu ya kwanza inaisha hakuna aliyeona lango la mwenzake. Ndipo katika dakika 15 za pili mwamuzi akamuonyesha kadi nyekundu mchezaji wa Azam baada ya kumchezea madhambi Ally Ufudu.
Katika penati alianza Mohammed Hassan akakosa, akafuata Hammad Juma, Mohammed Hassan Omary, Bakari Mwaita na Mwaita Salehe wote wakapata. Lakini kulitokea sintofahamu baada ya Mwaita Salehe kupiga penati na kukosa lakini mwamuzi akasema irudiwe baada ya golikipa wa Azam FC kutoka kabla penati haijapigwa, ndipo akapata lakini haikusaidia kitu kwani mchezaji wa Azam aliyepangwa kumalizia penati alipata.
Kwa matokeo hayo Azam FC watacheza fainali na Eagle Rangers ya Tanga, huku mshindi wa tatu Coastal Union watashuka dimbani dhidi ya JKT Oljoro waliofungwa mabao 2-1 na Eagle Rangers.
Hata hivyo baada ya mpira kuisha wachezaji wa Coastal Union waliingia kwenye bus lao kimya kimya ila wachezaji wa Azam FC waliokuwa wamejawa furaha ya ushindi walikuja kwenye Bus la Coastal Union na kuwakejeli huku wakiimba kwa nguvu. Wachezaji wa Coastal Union walijibu mashambulizi kwa kuwakejele ila mmoja wa wachezaji wa Azam alipishana kauli na mchezaji wa Coastal hivyo wakaanza kurushiana mawe.
Zilizuka vurugu kubwa kiasi mchezaji wa Azam, Gadiel Michael aliumizwa vibaya na kukimbizwa Hospitali. Hata hivyo viongozi wa michuano waliingilia kati na kuwataka Coastal Union wasiondoe bus lao mpaka atakapojulikana aliyempiga chuma mchezaji huyo.
Baada ya nusu saa polisi walifika uwanjani na kuwaita viongozi wa timu zote mbili ndipo ilipobainika ni Yussuf Chuma ndiye aliyempiga chuma mwenzake hivyo viongozi walimtaka kuomba radhi kwa mwenzake akiwa Hospitali.
COASTAL UNION
14 JULAI, 2013
ARUSHA, TANZANIA  

No comments:

Post a Comment