Wednesday, July 3, 2013

Mazoezi ya jumamosi iliyopita pia yalitumika kwa vikao vya hapa na pale kujadili mkutano mkuu wa jumapili.

 Hekaheka langoni mwa Coastal Union zilikuwa haziishi lakini golikipa alikuwa imara sana hakutaka mchezo.

 Ally Kiraka jamani anapenda kuongea, utafikiri amemeza radio.... Ahahaaaaa mwenyewe akinisikia!!

Hapo Mzee Bawazir ni kama anasema 'Mhh Siyo TD yule, hebu ngoja nikazungumze naye'
Hapa amemuona na anazungumza naye kuhusu usajili...
Baada ya kuzungumza na TD Bawazir akahamia kwa Shoka ni kama anamwambia 'Ebwana eenhh nimetoka kuzungumza na TID aahhaa nimekosea nimeongea na TD anasema anatuletea mchezaji kutoka Nigeria bwana... dah huyu jamaa ameamua mwaka huu.

Baki mbili yangu ya ukweli hiyo Coastal Union Hamad Juma 'Basmat' akionyesha uwezo wake. Kumbka Hamad alipandishwa msimu uliopita lakini kutokana na mapenzi ya timu ameamua naye kushiriki Rolling Stone.
 Ebwana eeenhhh sikuamini nilipokutana na beki wa kati wa Coastal Union Khamis Kibacha, huyu jamaa anajituma sana. Hapo amekuja mazoezini ingawa timu haijaanza mazoezi. Safi sana Kibacha.

Kuna historia huyu jamaa ameniwekea, nakumbuka tulipokuwa Bukoba msimu ulioisha baada ya kufungwa na Kagera Sugar, tuliporudi Hotel wakati tunazungumza na walimu pamoja na viongozi juu ya kufungwa kwetu mara akaja Kibacha huku analia. Aligomba sana huku akiwatupia lawama wachezaji wenzie kwa kucheza bila kujituma.

TD akiwa na msimamizi wa matokeo au kwa kimombo live uptade katika ukurasa wa facebook Ally Albusaidy wakionyesha uwezo wao kisoka.
Timu B inapendwa wewe....
Hapa ni viongozi watupu, namuona TD, meneja msaidizi Abdi Masamaki, Mwenyekiti Aurora na makamu wake Mzee Mnguto.

No comments:

Post a Comment