Wednesday, August 28, 2013

Bus la wachezaji Coastal Union lavunjwa vioo na mashabiki wa Ynaga, Hamad apasuliwa.

Sikuwepo wakati tukio hili linatokea, lakini niseme wazi kuna upendeleo mkubwa unafanywa kwa Yanga. Kuanzia vyombo vya ulinzi mpaka viongozi wa soka. Ninavyojua timu ngeni ndiyo inayopewa ulizinzi kabla na baada ya mechi. lakini leo imekuwa kinyume, limeanza kutoka gari la Yanga likiwa na ulinzi mkali wa FFU. Gari la Coastal Union lilitoka bila ulinzi, kufika maeneo nje kidogo ya wauanja wa Taifa likaanza kushambuliwa kwa mawe, watu kadhaa wameumia na aliyeumia zaidi ni Hamad Juma 'Basmat', ambaye alikuwa mwiba leo upande wa kushoto. Amepasuliwa kichwani na ameshona nyuzi kadhaa.

Nakumbuka mwaka jana mzunguko wa kwanza Yanga walikuja Mkwakwani wkatufunga 2-0, lakini kabla ya mchezo kuanza walirusha mawe mengi sana kwa mashabiki wa Coastal Union, baada ya mchezo kuisha wakaendelea kufanya vurugu hatimaye waliondoka uwanjani wakiwa na ulinzi. Angalia tofauti, vurugu wameanzisha wao na ulinzi walipewa wao, leo sisi tumeondoka uwanjani kimya kimya lakini pia tumevamiwa tukiwa hatuna uliznzi. 

Je huu ni uungwana?

COATAL UNION
28 AGOSTI, 2013
DAR ES SALAAM, TANZANIA

No comments:

Post a Comment