Monday, August 19, 2013

Yusuf Chuma Angara Mombasa.

Yusuf Chua akiwa mazoezini wakati alipokuwa akiichezea timu ya vijana chini ya miaka 20.

Kinda wa Coastal Union ambaye ni beki wa kati Yusuf Chuma, amewafungia wagosi wa kaya bao pekee katika mechi ya kirafiki ya kimataifa mjini Mombasa dhidi ya timu ya Admiral ambapo mechi hiyo iliishia kwa suluhu ya 1-1.

Mnamo dakika ya 78 kwa ufundi mkubwa kinda huyo aliyeshiriki michuano yake ya mwisho akiwa na timu B jijini Arusha, aliwainua mashabiki wachache wa Coastal Union ambao baadhi walisafiri na timu na baadhi ni wakati wa mji huo wa pwani nchini Kenya.

Kutokana na matokeo hayo kikosi cha Coastal Union ambacho kilitarajiwa kurudi leo jijini Tanga na kuanza safari ya kuelekea mjini Moshi watakapoweka kambi maka tarehe 24 jumamosi kwenye mechi ya ufunguzi wa ligi kuu tanzania bara, kinaonyesha dhahiri hakitaki mzaha baada ya kutoruhusu kufungwa kwenye mechi zote tatu za maandalizi ya ligi hiyo.

Viongozi na wanachama wa Wana Mangush wanaitakia kila la kheri timu yao kufanya vizuri kwenye ligi kuu ili kutimiza malengo ya mwaka huu ambapo vijana wa Tanga wanasema kauli mbiu ni Ubingwa.

COASTAL UNION
19 AGOSTI, 2013
DAR ES SALAAM, TANZANIA 

No comments:

Post a Comment