Saturday, August 24, 2013

Kikosi kitakachoanza dhidi ya Oljoro JKT leo.

                                        Umakini unahitajika wakati mwalimu anapozungumza.
Mwalimu Morocco akisisitiza jambo ubaoni. Kwa mbali majeruhi wawili Danny Lyanga na Jerry Santo wakimsikiliza mwalimu. Danny anasumbuliwa na kifundo cha mguu wakati Santo anasumbuliwa nyama ya nyuma ya ugoko (kigimbi).


 Yayo Kato akisikiliza kwa makini, ama kweli mpira unazungumza lugha moja dunia nzima. Yayo ni Mganda hajui kiswahili lakini alikuwa akimuelewa mwalimu.

Othman Abdullah akimwelekeza mwalimu kitu ambacho kwa upande wake hakuwa amekielewa vizuri. Huu ndiwo uzuri wa kuwa na mwalimu anayesikiliza wachezaji.



Kikosi cha leo kitakachoanza dhidi ya maafande wa JKT Oljoro katika uwanja wa kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid jijini Arusha ni hawa:
1  Shaaban Kado.
        Hamad Juma.
       Abdi Banda.
    Marcus Ndehele.
    Juma Nyoso.
       Razak Khalfan.
     Uhusu Suleiman.
        Haruna Moshi.
    Kato Yayo.
       Crispian Odula.
       Suleiman Kassim ‘Selembe’.

Sub: Said Lubawa, Mbwana Kibacha, Othaman Tamim, Pius Kisambale, Atupele Green, Yusuf Chuma na Mohammed Sudi.
Kwa maelezo a msisitizo kutoka kwa kocha amewataka wachezaji kupiga mpira golini ili kupata ushindi.

Ameongeza kuwa katika timu zote 13 zinazoshiriki ligi kuu hakuna hata timu moja inayoweza kuwazuia wana Coastal kushambulia.

COASTAL UNION
24 AGOSTI, 2013
ARUSHA, TANZANIA

No comments:

Post a Comment