Monday, August 5, 2013

Kocha wa timu B, Joseph Lazaro afiwa na mkewe.


 

Mke wa kocha mkuu wa coastal Union B, Joseph Lazaro amefariki dunia alfajiri ya leo katika Hospitali ya Bombo mjni Tanga baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Akitoa taarifa hiyo kutoka Tanga mwenyekiti wa hamasa Coastal Union, Miraji Wandi amesema mke wa Lazaro alikuwa akisumbuliwa na kiharusi (Stroke) kwa muda mrefu mpaka mauti yalipomfika saa tisa usiku wa kuamkia leo.

Kocha huyo ambaye amechukua mikoba ya aliyekuwa kocha wa timu B, Bakari Shime amesema msiba utakuwepo nyumbani kwake Makorora Mzingani na maziko ya kumpumzisha mkewe Bi Farida Mussa, yatafanyika leo saa kumi alasiri kwenye makaburi ya Maftah.

Joseph Lazaro pia aliwahi kuichezea Coastal Union na kuwa chachu ya mafanikio yaliyowafanya wana Mangush kuwa wafalme wa soka Tanzania Bara mwaka 1988.

Mungu ailaze roho ya marehemu Farida Mussa mahala pema peponi Amin.

COASTAL UNION

AGOST 5, 2013

DAR ES SALAAM, TANZANIA

No comments:

Post a Comment