Friday, August 23, 2013

HIKI NI KITUKO.....


Ahahahaaa Mara nyingine mambo huenda yakarudi, katika benchi wa pili kutoka kushoto ni Abdul mjukuu wa Mzee Abeid Msawa (Al Marhuum). Mzee Abeid ni African Sports wa kutupwa, humwambii kitu na Sports enzi za uhai wake. Ndiye aliyemfuatA Hussein Mwakuluzo, kumbembeleza arudi Sports baada ya kuhamia Coastal Union. Zikavuma habari kuwa Mwakuluzo alipewa Feni ili asajili Coastal. Lakini cha kushangaza huyu Abdul Msawa ndiye mwenyeji wetu Arusha. Hotel yake ndiyo tunayokula na timu nzima kuanzia chakula cha asubuhi mpaka jioni. Ila hakuna hujuma zozote na anadai yeye si kama babu yake yeye ni Coastal Union damu.

COASTAL UNION
24 AGOSTI, 2013
ARUSHA, TANZANIA

No comments:

Post a Comment