Saturday, January 5, 2013

Habari Picha Coastal inashika nafasi ya tatu katika msimamo... soma..

                                   Tamim na Selembe wakiwania mpira na mchezaji wa mtibwa....

Ismail Suma leo alikuwa haonekani kabisa hata sijui ilikuwaje... namba mbili ya nguvu hii...

                                               Kumi na moja ya nguvu Danny huyu jamani.


                                                    Mohammed Miraji 'Muddy Magoli'


 Nakumbuka zamani tukiwa wadogo mtu akiwa beki anajiita beki mkristo... Philip Mugenzi huyu namba tano ya uhakika ama kweli ni beki mkristo...

 Amani Makungu Mwenyekiti wa ZFA na mnazi wa Miembeni FC akisalimia wachezaji wa Mtibwa leo uwanja wa Amaan.

                                             Shengo hapa akitafakari ugumu wa game ya leo.

                                       Selembe na Santo wakitafakari kabla ya kuanza mchezo.



Kikosi Coastal Juma Mpongo, Ismail Suma, Othman Tamim, Mbwana Bakari ‘kibacha’, Philip Mugenzi, shengo, Selembe, Santo, Muddy Magoli, Muddy Sudi, Danny Lyanga.

Mtibwa: Hassan Sharif, Hamis Issa, Yusuph Nkya Salvatory Ntebe, Salum Swedy, Babuali Seif, Ali Mohammed, Rashi Gumbo, Hassan Seif, Hussein Javu na Vicent Barnabas.

Goli la Mtibwa lilifungwa dakika ya 58 na Ali mohammed, likakombolewa na Jerry Santo dakika ya 81.

Na katika mchezo wa pili uliochezwa uwanja huohuo wa Amaan saa mbil usiku kati ya Miembeni na Azam. Matokeo yalikuwa ni 3-1. magoli ya Azam yalifungwa na Joackim Atudo, Gaudience Mwaikimba na Uhuru Suleiman. Na goli la Miembeni lilifungwa na Adeyoum Saleh.

Kwa matokeo hayo kundi B litaongozwa na Azam waliokuwa na Point 4 magoli 3. ikifuatiwa na Miembeni waliokuwa na point 3 magoli 5, halafu Coastal Union point 2 goli 1 ikimalizia Mtibwa point 1 magoli 2.

Unguja, Zanzibar
costalunion@gmail.com
0713 593894
5/1/2013 

No comments:

Post a Comment