Monday, January 14, 2013

Kibacha ndiyo namba tano iliyowekwa katika kikosi bora katika timu 8 zilizoshiriki michuano ya kombe la Mapinduzi....

                                    Mbwana Bakari 'Kibacha' wa pili kutoka kushoto waliosimama.
Ngoja nikutajie kikosi kamili cha Coastal walio pichani: Mbele kabisa ni golikipa Juma Mpongo, Kutoka kulia waliosimama ni Jerry Santo (Nahodha), Suleiman Kassim 'Selembe', Danny Lyanga, Ismail 'Suma;, Shengo, Mohammed Miraji 'Muddy Magoli', Mohammed Sudi 'Mzee wa ugali', Philip Mugenzi, Mbwana Bakari 'Kibacha' na Tamim. Umenifahaaam?

Kibacha akisalimiana na mgeni rasmi katika mechi dhi ya Mtibwa sugar uwanja wa Amaan. ambapo mechi hiyo iliiishia kwa suluhu ya 1-1.


Hiki ndicho kikosi cha michuano ya kombe la Mapinduzi, si Haba Coastal tumeonekana tulikuwa imara sana katika nafasi ya ulinzi. Maana namba nne wetu ‘Kibacha’ amesifiwa kuwa ni beki mzuri wa kati na kawaida beki hasifiwi lakini huyu alisifiwa kutokana na umahiri wake ingawa hapa katika kikosi amewekwa namba tano ambayo katika Coastal Union alikuwa akicheza Philip Mugenzi.. Coastal twende.
1.   Abdul Swamad, (Miembeni).
2.   Himid Mao, (Azam FC).
3.   Adeyun Ahmed, (Miembeni).
4.   Salum Juma, (Miembeni).
5.   Mbwana Hamis Bakari, (Coastal Union).
6.   Khalid Aucho, (Tusker FC).
7.   Harun Athuman, (Simba SC).
8.   Humphrey Mieno, (Azam FC).
9.   Jesse Were, (Tusker FC)
10.   Haruna moshi, (Simba SC).
11.   Robert Omonuke, (Tusker SC)

chanzo: Mwananchi tarehe14/jan/2013 jumatatu.

No comments:

Post a Comment