Tuesday, February 26, 2013

Coastal Union hatihati mchezo wa kesho kuchezwa bila mashabiki.


Timu ya Coastal Union kesho itashuka dimbani dhidi ya maafande Ruvu Shooting kusaka point tatu muhimu zitakazoipandisha mpaka nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara.
Wagosi wa kaya wanacheza mchezo wao wa sita katika uwanja wa nyumbani wa Mkwakwani wakiwa na historia ya kupoteza mchezzo mmoja tu dhidi ya Kagera Sugar kwa kufungwa goli moja bila majibu katika uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.
Hata hivyo mgambo hao wa wanaotoka mkoa wa Pwani wameshaanza mizengwe kwa kukimbilia TFF wakidai mchezo uliopita katika uwanja wa Mkwakwani walifanyiwa vurugu na mashabiki wa wagosi wa kaya hivyo waliwasilisha malalamiko hayo kwa njia ya DVD wakionyesha tukio la vurugu kwa njia ya video, hivyo kuitaka TFF kuchezesha mchezo huo wa kesho bila mashabiki.
Hata hivyo shirikisho hilo la mpira wa miguu Tanzania haikutilia maanani malalamiko hayo hivyo mchezo wa kesho utakuwepo kama kawaida na tunawataka wapenzi wa Coastal Union kujitokeza kwa wingi ili kushuhudia timu yao ya nyumbani ikifanya maajabu na kuendeleza ubabe wa soka kutoka mkoa wa Tanga uliokuwepo kabla ya kupatikana uhuru wa Tanganyika.
Kwa kuthibitisha kuwa Coastal Union inawajali mashabiki wake wa nje ya mkoa wa Tanga mchezo huo wa kesho utarushwa moja kwa moja ‘live’ kwenye radio ya Kiss FM; pia kupitia ukurasa wetu wa facebook vijana wetu watakuwa wanaleta matangazo ya moja kwa moja kutoka uwanjani.
Coastal Union mpaka sasa imeshacheza michezo 18, na imebakisha michezo 8 ili kukamilisha michezo yote 26 ya ligi kuu. Na maombi ya viongozi na wanachama ni kuhakikisha wagosi wa kaya wanachukua taji hili ambalo wana uchu nalo kwa miaka 25 sasa tangu kulichukua kwa mara ya mwisho mwaka 1988.
Viongozi wa Coastal Union wakishuhudia timu yao ikipigwa 1-0 na Kagera Sugar uwanja wa Kaitaba Bukoba mkoani Kagera.

Aidha wagosi wa kaya wana point 30 kibindoni waking'ang'ania nafasi ya nne wakati Yanga anaeshika nafasi ya kwanza ana point 39, Azam FC walio nafasi ya pili wana point 36 na Simba wana point 31 wakiwa nafasi ya tatu.

ifuatayo ni michezo iliyobakia:

     27/02/2013 Mkwakwani (Tanga) Coastal Union Vs Ruvu Shooting.
2.    10/03/2013 Uwanja wa Taifa (Dar es Salaam) Simba Vs Coastal Union.
3.    16/03/2013 Manungu (Morogoro) Mtibwa Sugar Vs Coastal Union.
4.    30/03/2013 Azam Complex (Dar es Salaam) African Lyon Vs CoastalUnion.
5.     10/04/2013 Mkwakwani (Tanga) Coastal Union Vs JKT Ruvu.
6.     27/04/2013 Mkwakwani (Tanga) Coastal Union Vs Azam FC.
7.     01/05/2013 Mkwakwani (Tanga) Coastal Union Vs Young African.
8.     18/05/2013 Jamhuri (Morogoro) Polisi morogoro Vs Coastal Union.
 COASTAL UNION
costalunion@gmail.com
26 feb, 2013
Dar es Salaam, Tanzania

No comments:

Post a Comment