Monday, February 11, 2013

Tazama safari ya Coastal Union kutoka Mwanza kuelekea Bukoba leo jioni.

 Hapa ndiyo tunaiacha Mwanza tunaelekea njia ya feri Busisi, tuliondoka Mwanza saa tatu asubuhi leo.

 Hemed morroco na Juma Pondamali wakishuka kuingia ndani ya Feri kuvuka kuelekea Mwanza.

 Ally Kiraka nae alikuwemo katika msafara hapa akishuka kuingia katika feri.

 Mwenyekiti hapa akiwa ndani ya feri anasema hajawahi kuona ziwa Victoria maana ni kubwa balaa.

 Hapa vijana walishuka kuchimba dawa.

 Hapa panaitwa Katoro, leo kulikuwa na vurugu kati ya Waislam na Wakristo ambapo inasemekana wamekufa watu zaidi ya watatu. Vurugu zenyewe zilisababishwa na Wakristo wa eneo hilo ambalo lipo Mkoa wa Geita kuchinja mbuzi na ng'ombe kwa ajili ya biashara kitu ambacho kilikataliwa kisheria.


 Ilipofika saa nane mchana tulishuka sehemu moja inaitwa Muleba kupata chakula cha mchana. Muleba ni kilometa 70 mpaka kufika Bukoba mjini.

 Muleba hapa Selembe na Suma wakitembeatembea kuangalia mandhari na kushusha chakula.

Kutoka Mwanza kuelekea Bukoba ni kilometa 400, safari ilikuwa nzuri na tayari vijana wamepumzika tayari kwa mazoezi kesho asubuhi.

No comments:

Post a Comment