Thursday, February 14, 2013

Vijana wa Coastal Union wamewasili salama usiku huu.

Kikosi cha Coastal Union kutoka Tanga kimewasili jioni hii kutoka Mkoani Mwanza kwa ndege ya shirika la Fast Jet.

Wagosi wa kaya walitoka mjini Bukoba saa kumi za usiku kuelekea Mwanza ambapo walifika saa nane mchana na kupanda ndege saa kumi na moja na nusu jioni.

Ndege ilisafiri kwa saa moja na dakika kumi na tano, na kutua uwanja wa Julius Nyerere saa kumi na mbili na dakika 45 salama.

Vijana watalala magomeni, na kuanza safari kesho asubuhi kuelekea mjini Tanga kwa kuweka kambi tayari kukumbana na JKT Oljoro siku ya jumatano tarehe 20 februari.

Coastal Union ilicheza mechi mbili za kanda ya ziwa ambapo walitoka suluhu mechi yao dhidi ya Toto Africa mjini Mwanza na kupoteza mchezo mmoja dhidi ya Kagera sugar mjini Bukoba.

Coastal wataendelea kubakia nafasi ya nne wakiwa na point 27 mkononi, lakini wakiendelea kutoa suluhu ama kupoteza michezo iliyobakia kuna uwezekano wa kushuka nafasi za chini kitu kitakachopoteza hadhi yao waliyoanza kujijengea mbele ya wapenda soka.

COASTAL UNION
costalunion@gmail.com
14 Feb, 2013
Dar es Salaam, Tanzania.

No comments:

Post a Comment