Tuesday, February 26, 2013

Soma maoni ya mdau wa timu kuhusu mambo kadha yanayohusu timu.


Hongera "Coastal Union" na pia sitaacha kutoa maoni yenye lengo la kuijenga timu yetu kuwa yenye hadhi kitaifa na kimataifa.Mara nyingi tumeona"njaa ikiingia mlangoni,amani hutokea dirishani".Na sitapenda kuiona Coastal union ikizama kutokana na ukosefu wa fedha za uendeshaji.Moja ktk vitu muhim katika bishara kwanza ni bidhaa(product),ubora(quality),jina(brand),logo(nembo) na muhim customers(wateja/washabiki).
Vipi Coastal Union,imejiangalia katika hayo na mengineo kama yatakavyojitokeza wakati nikitoa /nikiwakilisha mada yangu.

Ningependa,wahusika wa mtandao huu kuiweka changamoto yangu kama ilivyo na ikiwezekana ipewe ukurasa maalum.

Nazungumzia Coastal Union(1948-2013),takribani miaka 65,changamoto za mwanzoni zilikuwa ni ushindani wa kijadi na changamoto za sasa ni ajira na biashara ili kuenzi urithi wetu.

Ili nisichoshe,naanza moja kwa moja na suala zima la bidhaa na hapa na maanisha soka,je! tumejiandaa vipi kwa ajili ya kuzalisha vipaji vipya(academy),kumiliki kiwanja yaani tuzalishe vipaji kwaajili ya kuchezea timu yetu nakuuza ili kupata fedha kujiendesha.Tusiwe wenye kupokea makapi toka Simba na Yanga(We dont need to buy classic ,we produce classic).

Umiliki wa Kiwanja ni muhimu,kwani miaka ijayo Mkwakwani Stadium kitakuwa na mechi nyingi na matamasha mengi kutokana na umuhimu wake.Timu kama African sports na nyengine nezo zinatumia uwanja huu kama wa nyumbani,matamasha na mikutano halkadhalka.Hapa yapasa uongozi uangalie faida ya kumiliki kiwanja kwani kijiografi inatuonesha utalipa kwa maana viingilio,ukodishwaji kwa matumizi ya biashara,matamasha,semina na mikutano.

Tukiangalia ubora(quality),hatujafikia kujiuza kutokana na soka safi na ushindani.Hapa itabidi,tujiangalie toka uongozi hadi kamati ya ufundi na timu yenyewe.Tuwe na viongozi wenye mawazo chanya na si hasi wasiwe viongozi mazoea wala kulindana.Tupate kocha anayejua timu inataka nini na wachezaji wanaojua majukumu yao.Kuwe na mkakati wa kuwa Simba na Yanga kama ndiyo soka la Tanzania ibaki kuwa historia.Tuna haki ya kuiwakilisha Tanzania kama tutatoa matokeo bora kutokana na soka safi na ushindani.

Ukweli Coastal Union,ni timu kongwe na jina lake linajiuza kitaifa na kimataifa haihitaji marekebisho ili kuendana na matakwa ya washika dau,tunaweza kama kutakuwa na mkakati madhubuti kuuza hisa.Dar Stock Exchange ipo pale,hebu uongozi ushirikiana na wataalamu wa kichumi miongoni wa wana Tanga au wapenda soka kuliangalia hili.

Kuhusu Logo(Nembo),hapa kidogo mtanisamehe kwani mimi binafsi juu ya kutoa ushauri sipo tayari kumvaa MBWA.Msingi wa kusema hivyo ni kuwa,Mbwa kama nembo ya timu ambayo inatumika kwenye vipeperushi ,jezi na fulana hata kofia inakuwa ngumu kujivika kivazi hicho kutokana na Imani ya kidini.Khofu yangu kuu,kuna watu wenye mtizamo kama wangu wanashindwa kutoa mchango katika timu kuhofia mgongano katika imani. 

Ningeomba kutoa changamoto kwa wadau na wapenzi wa Coastal Union kutafuta Nembo mpya na uongozi utoe fursa kwa wadau kuwakilisha zoezi hilo la utafutaji wa nembo mpya.

Unapozungumzia bishara haitakuwa na maana kama haikidhi wala haimfikii mlengwa.Mlengwa ni mtumiaji wa mwisho na ukizungumzia soka na maanisha wanachama na washabiki.Vipi Coastal Union inatumia fursa ilokuwa nayo kama timu pekee toka kanda ya Kaskazini yenye washabiki wengi ikizifata Simba na Yanga kwa kuwa na wananchama na washabiki wengi kitaifa.Uongozi lazima ulitambue hilo hakikisheni na mtumia ushawishi wa hali ya juu na kiutaalamu kuweza kujipatia wanachama wakutosha watakaoweza kulipa ada na kununua tiketi ikiwezekana za msimu mzima.

Mwisho ningependa Coastal Union kujithamini kama inaweza kujiuza na kukopesheka,inapasa kuwa na mtandao updated wenye kukidhi sifa na haja ili kuweza kutoa nafasi za matangazo ya kibiashara pia ni vyema kama Coastal Union ijisajili kama kampuni na ikiwezekana kumiliki television kuuza kazi zake kwani ni fursa njema kibiashara kwani nchi imetoka kwenye analogy na sasa ni digital hivyo ving'amuzi vitawawezesha kuuza mechi zenu ili kuonekana live na kuwafikia wadau.

Dunia ya sasa ni sayansi na teknolojia ikiwa Coastal Union hamjayaona hayo basi mtarajie teke litakalowajia.
Mimi Mdau wa Coastal Union
Ally Ahmad - asah04@hotmail.com

Ally Ahmad mnazi wa Coastal Union.
NB: Haya ni maoni ya mpenzi wa Coastal Union kutoka falme za kiarabu. Hata wewe ukiwa na maoni kuhusu timu basi huna budi kuwasiliana nasi kupitia email yetu costalunion@gmail.com.

No comments:

Post a Comment