Friday, February 8, 2013

Coastal Union kukabiliana na Toto africa kesho Mwanza. angalia picha za safari leo...

 Juma Pondamali kocha wa makipa akibadilishana mawazo na mzee wa timu katika msafara.

 Kushoto namuona Shaaban Kado, Ismail suma na Abdi Banda wakivuka barabara kwa Binslum.

 
 Ahahahaa miraji wandi akiiona hii picha atacheka sana, Hamad anapenda Basmat sana sasa leo Binslum aliamua kummaliza kabisa.

                         Vijana wa Coastal wakipata chakula cha mchana kabla ya safari.

 Mwenyekiti wa coastal Union Hemed Aurora akiwa na meneja wa timu akida Machai wakipata chakula.

Danny Lyanga akishuka katika gari mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Julius Nyerere.

                                         Barbosa akiwa na Phili uwanjani wakisubiri ndege.

 Walimu wote watatu Morroco, Ally Kidi na Juma Pondamali wakibadilishana mawazo uwanjani.

 Jembe na mimi nilikuwemo kwenye safara hapa nikiwa na jembe langu Selembe.

Nassor Binslum ambae ni mkurugenzi wa ufundi akitoa ahadi ya laki tatu kwa kila mchezaji ikiwa watarudi na point sita kutoka kanda ya ziwa. Yaani wakishinda mechi ya Toto Africa kesho na mechi nyingine dhidi ya Kagera Sugar tarehe 13 uwanja wa Kaitaba Bukoba. Lakini akawaambia wakishinda mechi moja kila mmoja atapata laki moja.

No comments:

Post a Comment