Thursday, February 28, 2013

Mwaka wa Shetani CoastalUnion......

Timu ya CoastalUnion jana ilishindwa kuutumia vema uwanja wake wa nyumbani kwa kulazimishwa sare ya bila kufungana na maafande wa Ruvu Shooting kutoka mkoa wa pwani.

Wagosi wa kaya walicheza mchezo wao wa sita katika mzunguko wa pili ligi kuu ya vodacom Tanzania bara ambapo mpaka sasa wana suluhu tatu, wameshinda michezo miwili na kupoteza mchezo mmoja.

kushindwa mechi ya jana kulimaanisha kitu kimoja tu kwa wapenzi wa mpira mijini Tanga, kunyimwa furaha ya kuwa nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi yenye timu 14. Hicho ni kitu wanachokingojea kwa hamu mashabiki wa wagosi wa kaya ambao wamesambaa duniani kote.

Wachezaji wa Coastal Union walioanza jana ni Shaaban Kado, Hamad Juma, Abdi Banda, Mbwana Kibacha, Philip Mutasela, Jerry Santo, Joseph Mahundi, Razakh Khalfan, Danny Lyanga, Rashid Hussein Simba na Suleiman Kassim 'Selembe'.


Baadae kocha Hemed Morroco alifanya mabadiliko na kumuingiza Mohammed Sudi na kumtoa Razakh Khalfan dakika ya 37 kipindi cha kwanza. lakini kufikia dakika ya 42 kabla ya kipindi cha kwanza kuisha nahodha wa Castal Union Jerry Santo aliumia kifundo cha mguu hivyo kulazimika kutoka na nafasi yake ikachukuliwa na Khamis Shengo.

hata hivyo kwakuwa jana Jerry Santo alionyeshwa kadi ya njano baada ya kumchezea madhambi mchezaji wa ruvu Shooting katika kipindi cha kwanza hivyo kukamilisha kadi tatu za njano, atalazimika kukaa nje mechi moja. Hivyo tutamkosa katika mechi dhidi ya Simba 10 March, 2013 uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

timu zilikwenda suluhu na ukame wa magoli yaani si Ruvu Shooting si coastal union walioona lango la mwenzie. Kipindi cha pili Coastal Union walionyesha udhaifu sana na kazi nzuri ya mlinda mlango wa wagosi wa kaya Shaaban Kado ilisaidia kuondoa aibu ya kufungwa nyumbani mpaka kufikia kupata heshima ya kuwa mchezaji bora wa mechi hiyo 'man of the match'.

kufikia dakia ya 54 alitoka Rashid Simba akingia Atupele Green lakini hakuna kilichobadilika mpaka kipyenga cha mwisho na hatimae wapenzi wa wagosi wa kaya wakatoka uwanjani na huzuni ya kukosa nafasi ya tatu inayoshikiliwa na wekundu wa msimbazi simba.

aidha mechi hiyo ya mwezi wa tatu uwanja wa Taifa itakuwa na ushindani mkubwa kwani ndiyo itakayoamua hatma ya Coastal Union kumaliza nafasi za juu.kwa maana Simba wana point 31 na coastal Union baada ya suluhu ya jana wana point 31.

COASTAL UNION
costalunion@gmail.com
28 Feb, 2013
DAR ES SALAAM, TANZANIA





No comments:

Post a Comment