Tuesday, February 26, 2013

Wakati leo tunajiandaa na mchezo dhidi ya Ruvu Shooting tuangalie maktaba yetu....

Hii ilikuwa ni safari ya timu kutoka Bukoba kuelekea Mwanza, tuliamka asubuhi sana watu walikuwa taaban. Unaweza kuwatambua hawa?

Hii ndiyo hali halisi ya maisha ya watanzania vijijini,hapa ni mkoa wa Geita tulishuka kuomba maji ili kutengeneza gari. Lakini tukakosa maji. Hapo wanatwanga muhogo ili wapike ugali wa mchana na mboga za majani.

Mwenyekiti kila wakati alikuwa anapenda kukaa peke yake ili aweze kutafakari majibu atakaayowapa wapenzi wa Coastal Union ni kwanini amerudi Tanga na point moja badala ya sita alizowaahidi.

Uzuri wa Tanzania ulinifanya kila wakati niimbe kimoyomoyo 'Tazama ramani, utaona nchi nzuuriii, yenye mto na mabonde mengi ya nafakaa....

Nimegundua mikoani ama vijijini nyota ya kijani haijapita. Kila unaepishana nae ana mzigo na mtoto mgongoni.

Selembe na Tamim walipopanda kivuko cha MV misuno walijiona kama wapo kwenye boti...
 
Hapa Bawazir anaonekana akitia fitna ili Bus letu lipate nafasi katika kivuko, maana tulikuwa nyuma ya muda. Tulipasa kufika Mwanza kabla ya saa sita ili tule na kupumzika kidogo maana tulitakiwa kufika uwanja wa ndege saa tisa alasiri. Lakini tulifika kivukoni saa sita mchana na kutoka kivuko cha Kigongo mpaka Mwanza mjini ni kilomita 45, si mbali sana ila gari ilikuwa mbovu inatembea kama jongoo.

Hapa ni nyuma kidogo, tulikuwa Mkoa wa Geita Katoro palipotokea vurugu za dini kuhusiana na nani achinje. Namuona waziri wa mambo ya ndani Dk Emmanuel Nchimbi alipotuona alitupungia mkono,maana nae ni mwanamichezo kabla ya kuteuliwa waziri wa mambo ya ndani alikuwa waziri wa michezo.

Nilipokuwa katoro niliagiza supu ya ng'ombe na chapati, si nikajisahau nikauliza nyama hii amechinja nani? Watu wote hotelini walinigeukia nikaonaa mmhhh mapanga yananihusu.

Kupumzika pia imo.

Jamani eenhhh kumbe mwalimu Hemed morroco kabla ya kuwa kocha alikuwa fundi magari, njia nzimagari alikuwa akitengeneza yeye, kwanza ilikuwa ikisumbua Battery, akaitengeneza na ilipokuwa inachemsha pia aliitazama rejeta na kuchokonoa vitu akamshauri dereva akifika Mwanza abadili rejeta.


Jembe nacheza kiduku,mtaitakaaa..

Maaaambo hayooo..

Hata sijui Mwalimu Ally Kidi alikuwa anamwambia nini Mbrazil wa watu Barbossa.

COASTAL UNION
DAR ES SALAAM, TANZANIA
costalunion@gmail.com
27 Feb,2013

picha zinaendele.......

No comments:

Post a Comment